ROHO YA UTASA

Somo: "Roho ya utasa" (Part A)

 Bwana Yesu asifiwe Sana!

Yohana 8-31-32
31  Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;
 32  tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.

Mpendwa ibilisi hatishwi na ulokole wako, hatishwi na kutembea na biblia, hatishwi au kujua nyimbo zote za kuabudu na kusifu au tenzi za rohoni.
Hakuna shetani anayeondoka katika maisha yako isipokuwa kwa kupingwa. Soma mwanzo mpaka ufunuo lazima apingwe ndipo aondoke,haondoki tuu hivihivi lazima apingwe. Mpingeni shetani naye atawakimbia. Ivyo Kuna vitu vya kufanya uvuke hapo ulipo. ndipo akuachie ibilisi, aachie maisha yako. Shetani haindoki tuu kwa kuwa wewe umeokoka. Au umeshiriki katika ibada. Shetani huogopa wewe kuijua kweli. Kuijua haki yako kupitia neno. Neno linasema nini kwa habari ya iyo haki iliyoibiwa? Yani kuzijua na kuzidahi haki zako ibilisi alizozozichukua, haki ya kufanikiwa kikazi, kibiashara, kuwa na kiwanja, kujenga, haki ya kuwa na amani, haki ya kusoma kufika mbali, haki kuwa na afya njema, haki ya kuwa katika ndoa, ya kuwa na watoto. Kama kwenu hakuna anayevuka form 4, ukijua kuwa mlifungwa na maagano ya kafara. Iyo ni moja pili sasa lazima uidai ile haki.

Yohana 15-7

7  Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

Kukaa ndani ya Yesu ni hatua moja, hatua ya pili ni maneno ya Yesu kukaa ndani yetu. Umeona formula ya kupokea. Wengi tuko ndani ya Yesu ndio tumeokoka lakini maneno ya Yesu hayapo ndani mwetu. Anasema Ombeni lolote mtakalo mtatendewa. Hoja nzito ni maneno ya Yesu. Kuna sehemu biblia inasema leteni hoja nzito tuhojiane tusemezane. Watu wengine hoja nzito wanapeleka mawazo Yao. Biblia inasema nawe utaijua kweli nayo kweli itakuweka huru. Biblia haijasema kweli itakuweka huru. Kitakachokuweka huru ni kitendo cha wewe KUJUA. Baada ya kujua ndipo sasa kweli itakuweka huru. Hicho ndicho shetani anaogopa.

Mungu ameongea nini kuhusu utasa?

Kutoka 23:26
26  Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza.
 27  Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao.

Roho ya utasa ni hali ya kutokifanikiwa katika kipengele flani kwa mda mrefu. Watu wengi wapo kwenye utasa na hawajijui kama wamefungwa katika utasa. Mungu hakukuumba ufanikiwe kidogo, Mungu hakukuumba uende kwa kuotea, Mungu hakukuumba uwe na matokeo madogo, Mungu hakukuumba ubahatishe, Mwanzo 1-27-28, ni mapenzi ya Mungu ufanikiwe. Maana kufanikiwa kwako kunamletea Mungu utukufu, kama hufanikiwi eneo lolote iyo sehemu Kuna utasa. Iyo roho ya utasa ikaa mahali hata ufanyaje huwezi kufanikiwa ni mpaka uivunje na udai haki yako kwa jina la Yesu ndipo utakapo ona matunda yakikaa. Ukitanuka, ukiendelea. Kama umefanya kazi mda mrefu mafanikio yako hayalingani Na kazi yako huo ni utasa, kama umefanya biashara miaka 10 huna hata nyumba ya kwako huo ni utasa. Utasa upo wa aina nyingi.

Aina za utasa
1. Utasa wa mwili- hukaa kwenye tumbo la uzazi-kutokuzaa huleta vimbe za tumbo hizi roho za utasa, mikono(uzalishaji wa mtu hutegemea nguvu ya mikono katika ulimwengu wa roho) miguu(miguu imepewa umiliki katika ulimwengu wa roho)
2. Utasa wa kibali(kutokukubalika, hata mazingira kutokukubali, maeneo kutokukubali hufanikiwi kwa lolote ilo eneo)
3. Utasa wa biashara(madeni, kufilisika, kutokupata wateja, kutokuuza)
4.Utasa wa kazi(kutokupata kazi, kufukuzwa kazi,kutokupanda cheo,kukandamizwa, kuchoshwa kufanya kazi)
5.Utasa wa mawazo,ufahamu (huwezi buni wazo la kuzalisha, kutegemea akili ya mtu mwingine,kufikia mwisho wa kufikiri, kushindwa kufanya maamuzi)
6. Utasa wa kiroho(kushindwa kuelewa neno, kusoma biblia, kushindwa kuomba, kushuhudia wengine, kubaki mtoto kiroho hukui kila siku, kutegemea kulishwa kila Mara kutafuniwa  kupewa, kwenda kwa hamasa na sio neno)
7. Utasa wa ndoa(ndoa haifanyi kazi pamoja na jitihada zote,malumbano yasiyoisha, ushindani usioisha,tatizo la mahusiano la mda mrefu lisiloisha hata baada ya jitihada zote)

Na mwingine mwingi...

Roho ya utasa huwa inasimamia wap?
1. Katika Kuzaa
2.katika kuongezeka
3.katika Matunda ya mwanzo yanaliwa hayawezi kujua

*kuzaa
mtu mwingine hazai faida au matunda mema, anazaa mapooza. Anazaa balaa, mikosi. Roho ya utasa inakaa sehemu kwenye mimba. Mimba Si ya mtu tuu. Mimba za kiuchumi. Mimba za ndoa, mimba za wazo la biashara, mimba ya kiroho,mimba ya uchumi, mimba ya mahusiano, kila kitu huwa kinaanza kama mimba katika ulimwengu wa roho. Mimba ya marafiki wema, mimba ya watu wa msaada katika maisha yako. Mimba ya biashara. Mungu anapoitunga tuu kama kitu au wazo.  roho ya utasa huja Na kuharibu iyo mimba. Watu wangap walipata mimba nzuri za idea au mwanzo mzuri gafla kama ni wazo. Au ni mtu. Au chochote ambacho kingesaidia mimba iyo kuzaa kinakufa. Piga picha katika maisha yako vitu vingap vimekufa mwanzoni? Na ulijua ni bahati mbaya? Au kawaida?


*Kuongezeka
Sasa mimba imeenda kwa misukosuko je swali litakuja itaongezeka? Ni ile mtu anasoma hapati kazi, ni ile mtu anafanikiwa kupata mtaji biashara haiendelei, ni ile mtu anafikia umri wa kuolewa alafu anakuja mtu ila haposi. Wanakuja  wanaondoka. Wanakuja wanaondoka. Iyo ni roho ya utasa.


*Matunda ya mwanzo yanaliwa hayaongezeki.
Hii sasa ndo ile tunaita kudumaza kitu, kama ni kitu kimevuka kuzaliwa, kimevuka kuongezeka sasa unahitaji Ayo mafanikio yakae mda mrefu hayakai. Unahitaji kwenda level za kimataifa, unahitaji kustaafu vizuri, unahitaji kuwa na security gafla matokeo Yale uliyopata Mara ya kwanza yanaondoka kabisa. Alafu inabaki stori. Alikuwa na hiki, alikuwa na kile.
Bwana Yesu asifiwe Sana. Kuna matunda ya watu wengi Sana ibilisi kayapukutisha na hayapo yamefutika.

Roho ya utasa imekalia watu wengi Sana na wanabaki kujiuliza kwanini siendelei, kwanini sivuki hapa. Tayari kuomba umeomba mlango umefunguka. Dalili zinaanza kuonekana gafla roho wa utasa anakuja kuharibu mimba. Kama mimba ikifanikiwa kuzaliwa utasa unakuja ili isiongezeke. Na kama itaongezeka basi matokeo ya kwanza utasa huzuia kwa kuyala Yale matokeo.  Au kuyapoteza ili mtu uyo abaki Na histori.

Jinsi ya kushughulikia roho ya utasa? Na maeneo gani makubwa roho ya utasa hukaa na kutawala maisha ya binadamu kwa robo tatu ya maisha ya mwanadamu. Fuatana nami kesho katika part B ya somo hili.

PART B

Bwana Yesu asifiwe Sana!

Yohana 8-31-32
31  Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;
 32  tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.

Ninyi mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu. Nyie mmekuwa wanafunzi. Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. Mpendwa Kuna kweli Mungu anataka uijue. Ili iyo kweli kupitia neno ikuweke huru.

Kwanini nizungumze kuhusu roho ya utasa? Jana kwanini Leo nizungumze kuhusu nyayo za miguu?

Mwanzo 25-24-25
24  Siku zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake.
 25  Wa kwanza akatoka, naye alikuwa mwekundu mwili wote kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau.
 26  Baadaye ndugu yake akatoka, na mkono wake unamshika Esau kisigino. Akaitwa jina lake Yakobo. Isaka alikuwa mwenye miaka sitini mkewe alipowazaa.

Wapendwa wengi utasikia wakisema Yakobo tapeli Yakobo tapeli. Bila kujua Yale yaliyoandikwa katika kitabu cha mwanzo 25-24..... Ni mambo ya ulimwengu wa roho. Nataka ungalie uhusiano wa nyayo zako za miguu na nafasi yako ya uchumi, nafasi yako ya ndoa, nafasi yako ya kufanikiwa, nafasi yako ya kuwa mtawala, nafasi yako ya kuwa msaada kwa wengine, nafasi yako katika ulimwengu wa roho Kuna uhusiano gani Kati ya nyayo za mguu na hatua za mtu? Au nafasi ya mtu? Nikurudishe hapo juu mstari wa 26, biblia inasema Yakobo wakati anazaliwa alimshika Esau kisigino! Manake nafasi ya uzaliwa wa kwanza haikuaanzia pale Esau alipobadilishana na chakula hapana. Ilianza pale tuu aliposhikwa kisigino. Manake Yakobo alichukua nafasi ya Esau tokea tumboni mwa mamaye Pale ndipo aliponyanganywa nafasi ayo uliyoyaona baadae ni matokeo ya rohoni. Ni kama vile wewe unavyoomba mambo yanaanzia rohoni kuja mwilini.

Kwa iyo Yakobo hakudanganya bali alikuwa anasema kweli alipomuambia Baba yake mimi ni mzaliwa wa kwanza alikuwa anamaanisha wala alikuwa hatanii.ile ilikuwa ni lugha ya kimamlaka lugha ya ulimwengu wa roho ndio mana kule chini ukiendelea kusoma mlango huo Mwanzo 27-18-29.....hata Baba yake baada ya kugundua alishindwa kufanya kitu sababu ya lugha ya ulimwengu wa roho inamamlaka. soma hiyo stori iyo, ISAKA alimuuliza mara mbili Yakobo maana alikuwa haoni akamuuliza lakini kweli wewe ni Esau mzaliwa wangu wa Kwanza? Akasema ndio, akamwambia nisogelee nikuguse maana Esau alikuwa na manyoya kwenye mikono. Na Yakobo alivaa ngozi yenye manyoya mikononi, Isaka akasema mwili huu ni kama wa Esau lakini sauti ni kama ya Yakobo. Pamoja na kuwa na daught Isaka hakuweza kufanya lolote na akambariki, na hakuweza fanya lolote sababu Yakobo tayari alichukua nafasi tokea alipomshika Esau nyayo za miguu ya Esau. Katika ulimwengu wa roho.

Yote yaliyoonekana nje ulikuwa ni utiisho wa ulimwengu wa roho,Maana utawala na hatua na nafasi ya mtu ipo katika nyao za mguu. Nyayo tunazozizungumzia hapa Si nyao hizi unazoziangalia kwa macho na damu zipo nyayo katika ulimwengu wa roho ambazo zimepewa mamlaka. Ndio mana wachawi wakitaka usifanikiwe katika hatua zako zozote Wao wanacheza na nyayo zako, wanachukua sehemu ulipokanyaga, au kutuma ma urgent wakikushika tuu tayari wameacha madhara ndo mana mambo ya Mungu yanatambulika rohoni. Kwa macho ya kawaida watasema aaah uyo mshamba mfano kusuguliwa miguu, kuoshwa miguu ni hatari wala si kwamba mimi ni mshamba sababu anayekusugua miguu hujui hata historia yake, hujui ukoo aliotoka , hujui wametokea ufalme gani? Wa Giza au wa Mungu. Wengi wanaopenda kupendeza watalipinga jambo hili. Ila baada ya kuwa tasa katika mambo flani flani kwa mda mrefu ndipo ataelewa haya mambo ya rohoni. Nyayo Maana zimebeba nafasi, zimebeba hatua zako, zimebeba mamlaka ya kutiisha falme za Giza, mamlaka za Giza, wakuu wa Giza.

 Mpendwa kila mahali unapoishi lazima Kuna falme za Giza za huo mtaa, Kuna wachawi wa huo mtaa, Kuna mizimu ya huo mtaa, Kuna jeshi la pepo wa baya huo mtaa, Kuna wanga, Kuna wasoma nyota, Kuna ma urgent wa kuzimu bahati mbaya wanatembea katika maumbo ambayo wewe ushayazoea kuyaona ivyo Si rahisi kuwagundua kama huna Neema iyo. Mtu akitaka kukufunga wewe kitu chochote usiendelee atadili na nyayo zako.

Luka 1:19
19  Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Anasema nimewapa mamlaka ya kukanyaga. Kwanini anasema kukanyaga? Kwanini hasemi kunyonga, ushawahi jiuliza? Kunyaga kwa sababu nyayo ndiyo zimepewa mamlaka,huwezi kukanyaga na mikono Bali nyayo, kukanyaga nyoka Na nge nyoka ni ibilisi mwenyewe katika ulimwengu wa roho, nge ni wale maurgent wa ibilisi mapepo mizimu, roho chafu, walinzi wa kipepo hao ndio nge, hizi ni lugha za ulimwengu wa roho, Bwana Yesu asifiwe Sana! Nataka uone uzito wa nyayo za miguu ili ujue kuwa nyayo zinabeba mamlaka, zinabeba nafasi, zinabeba hatua kwa iyo zimebeba roho tatu ya maisha yako.

Yoshua 3-15-16
15  basi hao waliolichukua hilo sanduku walipofika Yordani, na nyayo za makuhani waliolichukua sanduku zilipotiwa katika maji ya ukingoni, (maana Yordani hujaa hata kingo zake na kufurika wakati wote wa mavuno),
 16  ndipo hayo maji yaliyoshuka kutoka juu yakasimama, yakainuka, yakawa chuguu, mbali sana, huko Adamu, mji ule ulio karibu na Sarethani, na maji yale yaliyotelemkia bahari ya Araba, yaani Bahari ya Chumvi, yakatindika kabisa; watu wakavuka kukabili Yeriko.

*Biblia tena neno nyayo zimetumika kutiisha maji yakagawanyika. Biblia inasema makuhani wa Mungu walipokanyaga walipotia nyao zao ukingoni maji  yalitengeneza njia na wana wa Israeli wakapita. Na ukiendelea kusoma utaona kuwa ilibidi wale makuhani wasiondoke mpaka wote wamevuka mto Jordani. Tunaona nguvu ya utiisho katika nyayo.Bwana Yesu asifiwe kama jinsi nyayo za mtu zilivyokuwa na uwezo na mamlaka ya kutiisha falme za Giza, mamlaka za Giza kama jinsi Esau alivyonyanganywa haki zake kwa nyayo ndivyo jinsi nawewe pia unaweza kunyanganywa nafasi yako tokea mimba yako ilipotungwa kwa kupitia nyao. Au kuguswa nyayo zako, kwa njia yoyote na mitego yoyote, ibilisi anajua siri hii ndio maana anamiliki hatua za watu na watu wanakuwa na utasa, utasa wa hatua mchawi akitaka usisonge mbele, usitoboze anakuwahi kwenye nyao. Watu wanaona ni fashion kuosha miguu lakini hawajui jinsi wanavyoharibu maisha Yao, hawajui jinsi wanavyouza nafasi zao, hawajui jinsi wanavyoondoa mamlaka zao za kutiisha. Ili uishi kwa amani ni lazima hapo unapokaa wewe uwe juu ya wachawi, wanga, wakuu wa Giza,wachawi falme na mamlaka za Giza usije sema mtaani kwetu hakuna wapo. Kwa iyo utiisho wa hao ma urgent wa kuzimu upo kwenye nyayo zako katika ulimwengu wa roho. Na wanatesa watu, wanahangaisha watu. Watu hawasogei, hawaendelei, kumbe siri ndogo tuu ni wewe kuondolewa kwenye nafasi yako, wewe kuondolewa mamlaka yako, wewe kuondolewa hatua zako. Na unakuwa tasa. BWANA Yesu asifiwe Sana!

Ushahidi kwamba ibilisi hupiga hatua za mtu, mamlaka ya mtu, nafasi ya mtu kupitia nyayo.....

Ayubu 18-7-8
7  Hatua zake za nguvu zitasongwa, Na shauri lake mwenyewe litamwangusha chini.
8  Kwani ametupwa katika wavu na miguu yake mwenyewe, Naye huenda juu ya matanzi.

*anasema hatua za mtu zitasongwa,kwani ametupwa wavu katika miguu yake mwenyewe, naye huenda juu ya matanzi. Matanzi ni uchawi wa mafundo. Kuwekewa nyavu ni kutegewa mitego katika miguu ili usikimbie Kuna watu katika ulimwengu wa roho hatua zao zimewekewa Tanzi, zimewekewa wavu ndo mana anakuwa na utasa katika maisha yake. Vitu vinakufa, haziongezeki, matunda ya kwanza nayo yanakufa.

Maombolezo 4-18
18  Wanatuvizia hatua zetu, Hata hatuwezi kwenda katika njia zetu; Mwisho wetu umekaribia, siku zetu zimetimia; Maana mwisho wetu umefika.

*wametuvizia katika hatua zetu, hata hatuwezi Nenda katika njia zetu. Mwisho wetu umekaribia. Bwana Yesu asifiwe Si Mimi ni biblia inaongea maneno haya, hatua inamaanisha miguu. Miguu ndiyo inayofuata njia. Ndo mana mwisho anasema maana mwisho wetu umekaribia. Wapendwa watu wengi Sana wamefungwa hatua zao, wamechukuliwa nafasi zao wengine wamekuwa omba omba, ma house girl kumbe nafasi zao zimechukuliwa kupitia nyao. Wengine wanamekuwa ma professor lakini Si vya kwao wamechukua nafasi za watu. Mpendwa huwezi kujua Mungu alikupa nafasi gani hapa duniani na uyo unayemwomba msaada pengine alichukua nafasi yako kwa kujua au kutokujua. Halleluyah! Au uyo anayeuza aliyefanikiwa pengine alichukua nafasi ya hatua zako, mamlaka yako ya kutiisha kwa kupitia nyayo, ulimwengu huu ni wa mapambano anayeshinda ndiye anayemiliki. Bwana Yesu asifiwe Sana.

Baada ya kuelewa mpaka hapa sasa tunafanyaje?

*Damu ya Yesu ya kwenye miguu iliachiliwa ili wewe urudishe nafasi yako katika ulimwengu wa roho, ya kutawala, ili upige hatua, ili uwe na mamlaka katika nyayo zako. Bwana Yesu asifiwe. Inawezekana umekamatwa toka tumboni mwa mama yako kama Esau, au wamechukua alama za nyayo zako, kwa kujua au kutokujua. Hata ukawa tasa kiuchumi, kindoa, kazi, biashara, kiroho, kujenga, ukawa tasa kila mahali. Hufanikiwi umezungukwa na utasa kila mahali. Pengine ulikamatwa kupitia ardhi ya kwenu, kupitia uchawi, unahitaji ukombozi wa miguu kipengele cha nyayo. Ukombozi ni kila siku. Hasa baada ya kujua siri kubwa kama hii. Katika ufunuo 10-1-5 tunaona malaika wa Mungu alipotaka kumpiga ibilisi mguu mmoja aliuweka katika bahari, kwa kumaanisha kutiisha mamlaka za bahari. Mguu mwingine aliweka katika ardhi kwa kumaanisha kutiisha mamlaka za ardhini wachawi, mizimu na mikono akainyoosha juu kwa kumaanisha kumiliki mamlaka za anga. Vitu muhimu Sana hivi kujua mpendwa. Soma mwenyewe. Kwa iyo la kufanya omba rehema kwa nafasi ulizopoteza kama Esau, mamlaka ulizopoteza, na hatua zako zilizofungiwa tanzi, na kutegewa wavu. Kisha achilia damu ya Yesu ya miguuni . Ukiunganisha damu ya Yesu ya miguuni. Ukiachilia katika nyayo zako. Fanya ukombozi huo katika nafsi hizi zilizopotea aidha unazijua au huzijui. Fanya ukumbozi katika mamlaka zilizopotea, na hatua zako zilizo zongwa kwa utasa. Unganisha mambo hayo kwa damu ya Yesu ya miguu na  ukombozi huo. Fanya deliverance ya kumaanisha(self delivarence) utaanza kutembea tena, kumiliki nafasi yako tena,na kutawala tena.

Nawe utaijua kweli. Na iyo kweli itakuweka huru.


JINA LAKE MUNGU LIBARIKIWE!

 *kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu


josephntandu@gmail.com,0713297066

Comments

Popular posts from this blog

MAOMBI HATARI YA KUVUNJA UCHAWI WA MAFUNDO

MAOMBI YA KUFUNGUA KIBALI CHA  NAFASI YA KAZI

MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA KUCHELEWESHA