PART B-MFAHAMU ROHO MTAKATIFU VIZURI ILI UPATE MSAADA KATIKA NJIA ZAKO ZOTE


Bwana Yesu asifiwe! 

Part B tutacover maeneo manne

*Dhumuni la Roho Mtakatifu

*Faida/kazi za Roho Mtakatifu

*ninampokeaje Roho Mtakatifu

*Nitajuaje Nina Roho Mtakatifu

DHUMUNI LA ROHO MTAKATIFU

.kuwa msaidizi

.kuwa pamoja na wewe

.kuwa rafiki

Roho Mtakatifu haji kuharibu mipango yako. Roho Mtakatifu huja kufanya hizo kazi tatu. Roho Mtakatifu huja kukusaidia wewe kutimiza kusudi la Mungu. Tatizo laWakristro

wengi waliokoka hawajui kusudi Lao kwa Mungu. Kila mtu anakusudi aliloletewa hapa duniani. Iyo ni shule ingine sitaigusa Leo.Kwaiyo sababuhawajui kusudi au wako nje ya kusudi Roho Mtakatifu

wanamtumia sehemu moja tuu. "katika ibada" katika maisha mengine ya kawaida hawamtumii. Roho

Mtakatifu kazi mojawapo ni kukusaidia wewe kufanikisha huo mpango wako. 

Haji kukuharibia mipango yako.Watu wengi wanafikiri wakimkaribisha Roho Mtakatifu atakuja kuharibu mipango Yao. Matokeo yake wanamfungia nje alafu wanakomaa wenyewe. Wamesahau lile neno "hamwezi neno lolote pasipo huyo Roho.

Bwana Yesu asifiwe.

Yohana 15:5

. Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

*nataka nikufungue macho maana ya ilo neno na ukiijua hii siri haitakutoka moyoni mwako wala hutakaa husahau na itakujengea imani utakayoenda nayo mpaka mbinguni. "kwanini Yesu alisema hamwezi neno lolote pasipo Mimi" ?Wote tunakumbuka nini kilitokea baada ya Yesu kubatizwa na Yohana ubatizo wa maji Mengi? Roho Mtakatifu alishuka juu yake. Na mbingu zilimfunukia.Yesu ni

Mungu binadamu hapa duniani kubatizwa ubatizo wa Roho Mtakatifu. Hata wale waliokuwa wanabatizwa na Yohana Mbatizaji walikuwa wanabatizwa kwa ajili ya ondolea la dhambi (maji) but ubatizo wa Roho Mtakatifu ulifanyika kwa Mara ya kwanza kwa Yesu. Kwa wengine ni chakula kigumu. Roho Mtakatifu akusaidie. Ni hivi baada ya kuokoka mtu hubatizwa kwa maji Mengi ili 

kukamilishahaki yote. Then kipo kitendo cha kujazwa Roho Mtakatifu Kwa Mara ya kwanza huo

ndio ubatizo wa Roho Mtakatifu. Bwana Yesu asifiwe. Wengine wanaita ubatizo wa Moto.

 Nakufundisha maandiko sikufundishi jambo jipya!

Yohana 1:31

. Wala mimi

sikumjua; lakini kusudi adhihirishwe kwa Israeli ndiyo maana *mimi nalikuja nikibatiza kwa maji.*

Yohana 1:33

. Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye

ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, *huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.*

SASA TUJE KWANINI YESU ALISEMA HAMUWEZI NENO LOLOTE PASIPO MIMI?

Tuangalie Roho Mtakatifu alipomshukia

Mungu-binadamu wa kwanza Yesu Kristo alifanya nini?

-Aligeuza maji kuwa wine

-Aliponya magonjwa

-Alifufua wafu

-Alitoa pepo

-Alirudishia  wasiona kuona

-Viziwi walisikia

-Alizuia upepo wa Bahari

-Alitembea

juu ya maji

-Aliwalisha watu maefu mikate na samaki wachache na wote wakashiba wakasaza

-Alifundisha neno kwa hekima haijawahi tokea hapa duniani

-Alijitoa uhai Na kujirudishia uhai

*Kama Yesu alifanya

Yote hayo kupitia Roho Mtakatifu kama yeye alimuhitaji Roho Mtakatifu wewe unamuhitaji Mara 100.na maana ya lile neno

Marko 16:17

. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu

watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

Marko 16:18

. watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.

Marko 16:19

Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu

*Hapa Yesu alikuwa anazungumzia Roho Mtakatifu. Bwana Yesu asifiwe Sana.manake mkiwa Na Roho yule yule ambaye Mimi nilikuwa naye mtafanya haya na zaidi ya haya.

Yohana 16:7

. Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu.

*Mimi nisipoondoka huyo msaidizi hatakuja kwenu. Kwanini Yesu alizungumza haya maneno? Jibu its simple

Yesu alimpokea Roho Mtakatifu wote. Na

alipompomkea alifanya kazi aliyotakiwa kuifanya. ila tatizo la Yesu ilikuwa liko hapa.

.Mda

.Mazingira(eneo)

.jinsi ya kujigawa kila mahali

.Jinsi ya kumuhudumia kila mtu

.Jinsi ya kumfundisha Kila mtu

.watu waliomuamini walikuwa wengi Sana

Wote wanamuhitaji! Na yeye anahitaji awahudumie wote

Yesu akapiga hesabu siwezi kuwa Africa the same time niwe America au Ulaya nipite kila mahali niponye!

Nifanye muujiza! Nifundishe akaona simple way ni

kufanya kazi Kwa kila mmoja kupitia Roho Mtakatifu. Ndio maana ile sheria ya Musa zile amri 10 zipo moyoni mwako uwe umeokoka au hujaokoka unazijua.

Kwa iyo 

sasa Yesu ana Roho Mtakatifu alimchukua (whole from heaven) sasa kwanini Yesu alisema inanibidi Mimi niondoke. It's simple Roho Mtakatifu alikuwa ndani ya

mwili wa Mtu mmoja tuu ambaye ni

Yesu. Kwa iyo kusudi atoke ndani yake aje kwetu lazima amtoe kwenye mwili kwa kumtoa kwenye mwili kwa yeye kuondoka

kurudi katika UUNGU yani (Roho) Kwa iyo Roho Mtakatifu Atahitaji mwili tena wa

binadamu ili aendelee Ku operate hapa duniani. Ivyo ndio maana akawambia

wanafunzi kaeni humu ndani msiondoke mpaka aje Roho Mtakatifu awavike uwezo. Yani uwezo uleule aliokuwa nao Yesu. Bwana Yesu

asifiwe Sana. Kwa iyo

Sasa kwa kufanya hivyo Yesu tayari amesolve matatizo Yale pale juu. Anaweza kuponya akiwa Africa na America at same time. Anaweza kufungua watu akiwa Asia

na Europe at same

time. Maana tuko wakristo waliokoka na kujazwa Roho Mtakatifu zaidi ya 1bil sasa. Kwa iyo tatizo la Muda. Tatizo la mazingira. Tatizo la

kujigawa! Tatizo la usafiri amelisolve sasa badala ya Roho

Mtakatifu kutumia mwili mmoja wa Bwana Yesu anatumia miili bil 1 kufanya kazi zilezile za Yesu. Manake ni

Nini huhitaji Yesu akufuate nyumbani kwako kama Lazaro maana yupo moyoni mwako. Huhitaji

Yesu aje akufundishe habari ya hukumu haki Na dhambi yupo

Moyoni mwako kwa iyo huhitaji kufanya jambo kisha jiuliza hii ni dhambi au sio dhambi no hiyo unaijua vizuri. Iyo unaifahamu vizuri. Bwana

Yesu asifiwe.

Na ndio maana Yesu akasema hivi

Yohana 16:8

. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.

Ona hapo juu Yesu alikuwa anajizungumzia yeye.

Ona hapa chini pia

Yohana 16:16

. Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni; na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.

Ushawahi jiuliza hii manake yake nini? Maana yake ni hii mda si mrefu hamtaniona

katika mwili. Mda si mrefu mtaniona Katika mioyo yenu. Kwa iyo

Ni kweli ule usemi unaosema Jesus never say goodbye. Yesu hajaondoka. Anatawala kupitia Roho wake Mtakatifu. Ni Roho huyo huyo

Mtakatifu aliyekuwa naye Yesu

ndie kawachia wanafunzi wake. Na ndio huyo huyo anayeishi ndani yako. Bwana Yesu asifiwe Sana

SASA TUNAPOSEMA ROHO MTAKATIFU NI MSAIDIZI TUNAMAANA GANI?

*Roho Mtakatifu Ni Mungu sio kijakazi. Watu wakisikia msaidizi kinachowajia kichwani mwao Ni picha ya Housegirl

/houseboy. Kumbuka zile kazi za Yesu

alizokuwa anazifanya. Tofauti ya

Yesu Na wanafunzi wake wakati ule ilikuwa Ni nini? Ilikuwa Ni "Roho Mtakatifu" kwa iyo Roho Mtakatifu humtumikishi Bali yeye

Anakutumikisha, Roho Mtakatifu humwagizi Bali yeye anakuagiza, anachokuja

kukifanya ni kukusaidia kufikia malengo yako, kuwa Na malengo au kujua

Kusudi la Mungu haina maana umefanikiwa no! no! no! Bado unamuhitaji Roho Mtakatifu akusaidie. Kwanini unamujitaji Roho

Mtakatifu

akusaidie ni sababu yeye ni Mungu anavyovitu vya kukusaidia ufanikiwe kwa wepesi ambavyo wewe huna. Bwana Yesu asifiwe. Unaweza kuwa na pesa za

kujenga kiwanda na idea ya product lakini haina maana tayari umefanikiwa bado utahitaji wataalamu wa sheria, wataalamu wa mazingira, wataalamu

utawala, wataalamu wa uhasibu, wataalamu wa manunuzi, utahitaji engeneers, wa chemicals! Na

industrial mechanical, utahitaji wataalamu wa store,

utahitaji wataalamu wa mauzo, tena ukiwa umeokoka Una hofu ya Mungu utahitaji watumishi wa kuja kuombea eneo lako kabla ya ujenzi hata baada ya

ujenzi. Wataalamu wa Muundo au designers wa jengo, yani bado unahitaji vitu vingi. Sasa Roho Mtakatifu Ni Mungu

ambaye anavitu vyote hapo juu na vya ziada. Ukimpata Yeye umepata vyote. Bwana Yesu asifiwe Sana! Na ndio maana ya lile hamwezi lolote pasipo mimi

.Roho Mtakatifu Ni mbunifu

.Roho Mtakatifu Ni mzalishaji wa vitu yeye ndio anayetoa Rohoni kuja mwilini

.Roho Mtakatifu ana hekima ya

hali ya juu

.Roho Mtakatifu ana maarifa ya hali ya juu

.Roho Mtakatifu ana ufahamu  hali ya juu

.Roho Mtakatifu  ndo anaye multiply vitu

.Roho Mtakatifu   anaona vitu vya Rohoni

.Roho Mtakatifu ana

sensitivity ya hali ya juu yani manake ana predict kinachokuja

Iyo ni mifano michache tutaingia ndani kule mbele. Kwa iyo unachohitaji wewe ni plan. Ukiwa na plan yeye anakuja kukuonyesha jinsi ya

kuimpliment. Watu

hawaelewi kwanini Mungu anaweza kukuonyesha mwanzo na mwisho wa jambo jinsi itakavyokuwa. Mfano nini kusudi lako? Kusudi Langu hapa duniani ni

kufundisha neno la Mungu. Nini maono

yako? Maono yangu ninaona ipo siku nitafundisha watu laki 3 kwa Mara moja. Lakini utafikaje katika maono yako don't

worry iyo anayo Roho Mtakatifu anayo jinsi ya kufika. Mungu anakuonyesha wewe ni

tajiri Sana ni kweli huko ni mwishoni but katikati hapa pana Roho

Mtakatifu. Mungu anakuonyesha unabiashara kubwa, umeolewa, anakuonyesha katika ndoto mambo mazuri well and good hapa Katikati Una

Muhitaji Roho Mtakatifu. Mungu amekutolea unabii kupitia Nabii thank you Jesus but unahitaji vitendea kazi! Vitendea kazi anavyo Roho Mtakatifu

Kwa iyo Roho Mtakatifu hakwepeki. Unaweza kukomaa

kufanya mwenyewe sikatai lakini mwisho wake utafika umechelewa Sana, umechoka hata haina

Maana tena maishani mwako, bila Roho Mtakatifu utakata tamaa! Sababu mwenye hekima za kupita kwenye Hilo

tatizo kirahisi ni Roho Mtakatifu sio

wewe. Mwenye maarifa ya kuondoka kwenye ilo tatizo ni Roho Mtakatifu sio wewe, mwenye ufahamu ya mambo ya Rohoni na mwilini ambayo unayatafuta

maisha yako yote

ni Roho Mtakatifu. Kwa iyo Roho Mtakatifu anavyovifaa vya kazi vya kukufanya ufike kwa wepesi kule unakoenda. Bila kuchoka. Na saa ingine

ukifanya kila kitu wewe unachoka unakata tamaa unaamua

kuachana navyo. Tatizo la binadamu akisoma kidogo anafikiri amepata vitendea vyote vya kazi vya

Kutatua matatizo. Kwa iyo Roho Mtakatifu Ni mtatua matatizo katika mipango yako. Roho Mtakatifu ni

mwondosha changamoto katika mipango yako. Roho

Mtakatifu ni mwezeshaji katika mipango yako. Roho Mtakatifu ni mtiaji nguvu katika mipango yako nguvu zote, nguvu za mwili, nguvu za akili, nguvu za kiuchumi

Nguvu za maarifa, nguvu za hekima, nguvu za ufahamu juu ya jambo flani. Bwana Yesu asifiwe Sana. Roho Mtakatifu ana vifaa vyote vya kazi vya kuhakikisha

Umefikia maono yako kwa iyo ni

msaidizi Roho Mtakatifu. Jina la Bwana libarikiwe.

Zaburi 32:8

. Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.

TUNAPOSEMA ROHO MTAKATIFU KUWA PAMOJA NA

WEWE TUNA MAANA GANI?

Manake ni hii! Wazungu wanaita companion yani unaweza kusikilizana na mtu lakini asiwe pamoja na wewe. Unaweza kuishi na mke au Mme ndani

Lakini asiwe pamoja na wewe. Laiti

Mungu angekufunulia mioyo ya watu uangalie jinsi inavyokuwazia ungeshangaa Mme anaweza kukupenda au mke

na kukuhudumia lakini ikifika maamuzi flani akakataa kuwa pamoja na wewe. Mfano kitendo

mwanaume kuleta ndugu zake ndani ya nyumba ingawa anampenda

Mme wake mke anaweza asiwe pamoja Na yeye. Utasikia mtu anasema  "kwa ilo siko pamoja na wewe kabisa". Mke anaweza anzisha maneno maneno
mtaani

Kwa kukosa hekima labla akasababisha watu wakatenga. Case ikaja kwa Mme wake akamwambia mke wake Katika hili sipo pamoja na wewe. Au mke kwa wivu

tuu akajikuta ameuwa mtu kwa tetesi tuu hapo

Mme wako akamwambia katika hili upo mwenyewe sipo pamoja na wewe. Bwana Yesu asifiwe Sana. ROHO

MTAKATIFU Ni mtu pekee anayeweza kuwa pamoja na wewe no matter what! Anaweza kuwa pamoja na wewe ukiwa

gerezani! Au watu wote wamekugeuka Na

Kukucheka au wamekukimbia Roho Mtakatifu atakuwa pamoja na wewe. Roho Mtakatifu atakuwa pamoja na wewe hata kwenye mambo madogo Sana mfano

Unajaribu kuwaelezea

watu kitu Na wanakubishia Roho Mtakatifu atawafanya wale watu wakusikize. Roho Mtakatifu Hata kwenye mpira atakuwa pamoja na

wewe.atashangilia na wewe Unajua interest zinatofautiana Kati ya mtu na

mtu. Mfano Mme anaweza kuwa anapenda mpira mke hapendi mke

anapenda kwenda kutembea kutoka out

Kuna vitu ambavyo huvipendi na ambavyo unavipenda binadamu ana limit Sana Katika vitu ambavyo havipendi 

anaweza kukutenga kuwa mbali na wewe ila katika

Vitu ambavyo vina interest zake anaweza kuwa pamoja na wewe. Kwa iyo Roho Mtakatifu si mnafiki. Yeye yupo pamoja

na wewe no matter what. Hata kwenye

Kutenda dhambi yupo pamoja na wewe kukumbusha habari ya hukumu haki na dhambi. Na kukuletea huzuni na

kuhakikisha umekosa amani mpaka

Umetubu. Binadamu mpe nafasi Katika moyo lakini usimpe moyo

wako. Moyo wako mpe Roho Mtakatifu maana yeye

Hana upendo wa kinafiki. Binadamu wote wanahitaji mtu wa kuwa pamoja naye no matter what! Binadamu kwenye aibu atakukimbia! Binadamu kwenye

kuhukumiwa

atakukimbia! Binadamu kwenye fedheha atakukimbia! Binadamu kwenye matatizo atakucheka atafurahi! Atakuwa pamoja na wewe huku

anakungonga lakini si Roho Mtakatifu! No matter What! Roho Mtakatifu

atakuwa pamoja na wewe. Lakini sasa ninajua kwanini watu huwakimbia watu au

kuwapa migongo wakati wa matatizo. Ni sababu hawana tools za Roho Mtakatifu, yeye ana kumbatio, yeye anafariji, yeye

anarudisha tumaini, yeye anakuletea

tabasamu, uyo ni Roho Mtakatifu yeye ana kutia nguvu, yeye anakuombea, yeye anakutia moyo, yeye anakufungua macho no matter what! Kwa kweli ukimjua Roho

Mtakatifu you will fall in love with him. He is true companion. More than your husband, more than your wife, more than Friend, more than your Children. More

than your neighbour, hawa wengine

wanaweza kuwa pamoja na kwa mda tuu. But yeye Roho Mtakatifu yupo pamoja na wewe hata ukienda kuoga atakufuata ataanza kuongea na wewe! Unashangaa

ukimaliza kuoga jibu ulilokuwa unatafuta tayari

umelipata. Roho Mtakatifu Ni zaidi ya kiu ya maji. Ni kweli hatuwezi bila yeye. Ana tools zote binadamu anazozihitaji

hapa duniani. Zoote zipo kwake. Kuzipata lazima uambatane naye. Bwana Yesu

asifiwe sana. Roho Mtakatifu yupo pamoja na wewe.

TUNAMAANA GANI TUNAPOSEMA ROHO MTAKATIFU NI RAFIKI?

Rafiki ni mtu wa karibu ambaye mnaelewana na mko huru kushirikishana baathi ya mambo au mambo

yote. Kipo kitu kinachofanana ambacho kilishaabiana

ndani mwenu. Ambacho ndicho kilichowaunganisha. Kwa iyo urafiki huanzia moyoni kibali cha urafiki huanzia moyoni. Wako waliokuwa marafiki sababu

ya interest zao zimefanana. Mfano wote wanapenda mpira. Wote wana watoto mapacha. Au wote ni weupe wafupi. Au wote hawapendi mtu kuonewa, au wote

wanapenda neno la Mungu aidha Ni mazingira au Ni

sababu zimewakutanisha but lazima kuwe Kuna kitu kinaitwa common interest. Kwa saa ingine

unaweza kuwa huru Sana kushare mambo yako kwa uhuru au siri zako kwa rafiki kuliko mme au mke. Au ndugu au

wazazi. Rafiki saa ingine anaweza chukua nafasi

ya watu muhimu katika maisha yako. Na watu wasikuelewe. Bwana Yesu asifiwe! Kwa wewe na Roho Mtakatifu haina tofauti. Interest yako wewe ni interest

yake yeye. Kivipi?

Yohana 16:14

. Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.

Yesu anatukuzwa Katika maisha yako na anapopata sifa pale mtu anapoona ahadi za

Mungu zimekuwa kweli katika maisha yake. Baada ya mapambano ya mda

mrefu ukafikia ushindi wako ukamiliki kile ulichokuwa unaomba Yesu huwa anatukuzwa katika mdomo wako. Midomo ya waliokuzunguka.

Kwa iyo kazi

Ya Roho Mtakatifu Ni kuhakikisha kwamba Yesu anatukuzwa sasa Yesu anatukuzwa vip? Anatukuzwa kwa kukusaidia wewe upate unachotakiwa

Kukipata. Sawasawa na zaburi 32:8 Bwana Yesu asifiwe.

Sasa rafiki haiishi hapo tuu rafiki pia anaweza shear na wewe siri. Roho Mtakatifu huwa anashear na sisi siri

Yohana 16:13

. Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye

kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Katika vipengele ambavyo Roho Mtakatifu huwa nampenda kama

rafiki huwa always mambo yanayokuchanganya au mambo unapatashida kufanya maamuzi au

mambo usiyoyaelewa Roho Mtakatifu kazi yake atakutia katika kweli yote manake atakufunulia kila kitu. Yeye si ni

rafiki basi hufanya mambo kwako kwa mwingine

hawezi kufanya. Rafiki anaweza mkopa rafiki mwingine hata mil200 kwa kumuamini tuu. Bila hata dhamana ya kitu chochote sasa Roho Mtakatifu kwako

Ni zaidi

ya rafiki! Kwa iyo yuko tayari kukuibia siri za ufalme wa Mungu kukuambia. Yuko tayari kukutoa katika giza. Yuko tayari kukujulisha ukweli

Yuko tayari kukuambia yanayokuja. Mfano mimi nikitaka

habari zako sitazitafuta kwa watu nitachukua jina lako nitajifungia nalo ndani nakumuuliza Roho

Mtakatifu yeye atanifunulia kila kitu kuhusu wewe. Nikitaka kujua habari za uyu mtumishi nitajifungia

ndani nitafunga na kuomba na Mungu atanifunulia nitajua

Tatizo wengine wakijulishwa basi wanaanza kuropoka ukifanya hivyo Roho Mtakatifu hataongea tena na wewe. Unless amekuambia uongee kama

hajasema dont talk. Mfano mimi napokuwa Rohoni ninapoongea na wewe Roho Mtakatifu hudownload habari za mtu zoote kabisa. Ila siwezi kusema wala

Kukuambia tena ni mpaka Roho Mtakatifu aseme aruusu

Bwana Yesu asifiwe. Kwa iyo rafiki anaweza kukutendea mambo ya ziada ya wengine. Jina la Bwana libarikiwe

Kwa iyo tukitumia advantage ya urafiki wetu na Roho Mtakatifu utajikuta wewe unajua mambo

mengi. Una majibu mengi. Na mambo yanayokuja tayari unayajua

Hata yakitokea unajua kabisa Mungu aliniambia. Nabii wa kwanza wa maisha yangu mimi ni Roho Mtakatifu. Holly Spirit  is wonderful

atakupeleka chanzo cha

tatizo atakuleta kwenye situation uliyopo sasa na atakuambia nini cha kufanya. Bwana Yesu asifiwe. Uyu Bwana mkubwa kuwa rafiki yako ni sawa kuwa na tochi

Katikati ya giza

nene unaona kutambua kuelewa vitu wengine wanaona giza,  wengine hawana iyo tochi iyo ila wewe unayo. ingawa haya nayokuambia kuyapata lazima uwe

.mnyenyekevu

.Mtii

.uvumilivu

Roho Mtakatifu huwa hana

haraka. Yeye ni Mtaratibu. Na mstaarabu. Si kwamba anashindwa but akitumia spidi yake katika maisha yetu tunaweza tusi survive.

Sababu its most poweful being on heaven and on earth. Tatizo Roho

Mtakatifu tunamtumia may be 1% tena katika kusifu na kuabudu au neno la Mungu. But yeye

He is multpurpose anafanya vitu vingi sana beyond your thinking Bwana Yesu asifiwe.

FAIDA/KAZI ZA ROHO MTAKATIFU.....

1.kukuvika uweza utakao juu

Luka 24:49

. Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.

Uweza maana yake "ability to do" Mungu amekupa kila kitu kasoro uweza wa

kufanya hivyo vitu. Huo uweza ukiupata ndipo mambo yanaenda kwa wepesi

ndipo mambo yanaenda kwa uraisi Bwana  Yesu asifiwe. Timu ya mpira ina wachezaji 11 inakuwaje katika timu yote mastaa utakuta

ni wawili au watatu? Ni sababu 

wamevikwa uweza. Wa kuwa staa. Yani kwao kucheza mpira kukimbia kupiga chenga kufunga goli hawa struggle kama wengine kwao ni automatic! Sio kitu cha

kutafuta au

kujifunza kipo kwao automatic. Sasa huu uweza ukija sehemu mbalimbali za maisha yako ndipo unakuta mahali ulikuwa umekwama unapita kwa

wepesi. Uweza si kwa ajili ya kuhubiri injili tuu. Uweza

utokao juu unacover sehemu zote katika maisha Bwana Yesu asifiwe sana. Ukiona wewe unaenda hatua zako

kwa ugumu. Huna wepesi jua nyuma yako hakuna uweza ukusaidio. Uweza huu unaposhuka na unapovishwa basi utakuta mazingira yanalazimishwa kuwa upande

wako. Watu wote wanakuwa upande wako. Wakati watu wanaleta nyanya zao mfano sokoni hawauzi nyanya zinaoza ukileta wewe unauza zote na zinaisha na

watu wanagombania nyanya zako. Ukimaliza wewe ndipo wengine wanauza. Ukiona ivyo jua upo uweza uliovishwa juu. Yako na uweza ninaozungumzia hapa ni

uweza wa Mungu. Unakuta mtu anajaribu

kujenga nyuma miaka 7 na bado haijaisha ila wewe ile kuanza msingi tuu nyumba iyo iyo mara baada ya miezi mitatu nyuma

imeisha na kiukweli si kwamba ulikuwa umeweka akiba ila unashangaa tuu kila

ukitoa ela zinaingia nyingine. Kila ukitoa ela zinaingia nyingine unashangaa. Ukiona

ujue huo ni uweza utakao juu. Ukifanya kitu kwa struggle manake ni moja tuu haujavikwa uweza utakao juu.. Huu

uweza wa Kimungu unakusaidia kufanya 

unachokifanya ufanye kwa wepesi kabisa. Sasa mwenye kazi ya kuvika watu uweza ni Roho Mtakatifu. Bwana Yesu asifiwe! Sasa angalia hapa. Wanafunzi wa Yesu

walikaa na Yesu miaka 3! Wakijifunza pamoja na kujifunza kwa kuona na kupractice na imani yao kuwa kubwa sana Bado Yesu anawaambia no! Msianze kazi

Petro! Msianze kazi Yohana! Subiri Paulo mkishavikwa uweza utakao juu ndipo mtaweza. Uweza wa Mungu kazi yake ni kumsukuma adui nyuma ili wewe uweze

kupita. Uweza wa Mungu ukivikwa kila kitu kitalazimishwa kukutii. Na kuwa upande wako.

Uweza wa Mungu ni special nguvu za Mungu za kukusaidia ufanye kitu

flani kwa wepesi. Uweza huo ndo unamfanya mtu awe mwalimu wa kutegemewa. Doctor wa kutegemewa. Wakili wa kutegemewa. Uweza huo ndo

una mfanya mtu awe staa. Uweza huo ndo unamfanya mtu awe mwanasayansi hatari. Uwezo huo ndio unaomfanya mtu awe engineer wa kutisha. Uweza huu wa

kimungu ndo unamtofautisha mtu mmoja na mwingine

wanachokifanya. Mtumishi na Mtumishi. Mchezaji na Mchezaji. Msusi na Msusi. Kwa iyo ukiona unastruggle

eneo lolote katika maisha basi ujue hujavikwa uweza utokao juu katika ilo eneo.  Mungu kabla

ya kukuvika anangalia icho unachokifanya je alikuambia

ukifanye? Je ni mpango wa Mungu ufanye biashara? Je ni mpango wa Mungu ufanye kazi? Je ni mpango wa Mungu uwe Mtumishi kama ni mpango wa Mungu

katika ilo unalolifanya basi atakuvika uweza wake. Hii ipo hata kwenye ndoa kama ndoa ni ya Mungu basi Mungu atakupa uweza utokao juu maarifa na

hekima ya kuishi na uyo mwanamke na uyo mwanaume.

Bwana Yesu asifiwe. Kwa iyo hakuna ambacho hakivikwi uweza. Sasa kazi hii ni ya Bwana mkubwa ROHO

MTAKATIFU. Ndo mana Roho Mtakatifu ni Muhimu sana hapa duniani kuliko hata Roho yako. Watu wengi

sana wanaishi katika giza mateso na shida na taabu. 

Sababu hawamjui Roho Mtakatifu. Au wanamjua lakini wanamdharau. Kila kitu chako hapa duniani kimefungwa kimekuwa packed kwa Roho Mtakatifu.

Utaruka ruka tuu na kukimbia but kumkataa Roho Mtakatifu ni kumkataa Mungu. Kumkataa Mungu ni kujiangamiza. Bwana Yesu  asifiwe.

Yesu hajaondoka duniani bado yupo anatawala kupitia Roho

Mtakatifu.kutomtambua Roho Mtakatifu ni kutomtambua Yesu. Halleluyah

2. Msaidizi

Yohana 14:16

. Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine,

ili akae nanyi hata milele;

Yohana 14:17

. ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani
yenu.

Roho Mtakatifu

-anaona mambo ya Rohoni

-Anajua yote,ana majibu yote

-Ana nguvu na uweza wote

-Ni mbunifu

-Ana hisi vitu

-Anajua siri za Mungu

-Anajua yanayokuja

-Mtengenezaji njia

-Mnyooshaji njia

-Ni Muongezaji

-Mzidishaji

-Ana nguvu ya kuanza jambo

-Ana nguvu ya kuendeleza jambo

-Ana nguvu ya kumalizia jambo

-Ana nguvu ya kuumba tena jambo

-Ana nguvu ya kutowesha jambo

-Ana nguvu ya kurudisha jambo

-Ana nguvu ya kuwahisha jambo

-Ana nguvu ya kuchelewesha jambo

-Roho Mtakatifu muwezeshaji wa yote

-kukutengenezea mipango

-kukumbusha mambo muhimu

-Roho Mtakatifu ni mtengenezaji structure

- Roho

Mtakatifu ni muondoaji vikwazo

Kazi kubwa ya Roho Mtakatifu ni kuhakikisha kwamba jambo unalolifanya unalifanya bila kukwama kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Bwana Yesu. Yeye ni msaidizi katika

-kazi

-biashara

-ndoa

-Miradi

-Shule

-Huduma

Chochote unachokifanya kiongozee hapo kazi ya Roho yeye atakichukua mwanzo mpaka mwisho atakukabithi tayari kimekamilika alafu bado ataendelea kukufuatilia Bwana

Yesu asifiwe. Roho

Mtakatifu haji kukuvurugia mipango yako anakuja kuhakikisha kwamba mipango yako inasimama na inakamilika. Bwana Yesu asifiwe. Yeye ni rafiki, yuko pamoja na wewe. Yeye ni

msaidizi uyo ni Roho Mtakatifu.

3.Mwalimu

Zaburi 32:8

. Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.

Roho Mtakatifu

kazi yake kubwa kwa binadamu ni kumfundisha binadamu ili aweze kufanikiwa. Bwana Yesu asifiwe! Ile ministry ya kufundisha iliyokuwa ndani ya

Yesu ilitoka kwa Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu

atakufundisha kila kitu. Sijapata kuona mtu kama Roho Mtakatifu. Mtu ni nafsi ya Mungu. Bwana Yesu asifiwe

-Roho Mtakatifu atakufundisha kuishi na wakorofi

-Roho Mtakatifu atakufundisha jinsi ya kukaa na mme,mke na watoto

-Roho Mtakatifu atakufundisha jinsi ya kuishi na watu wasikukimbie

-Roho Mtakatifu atakufundisha kusamehe na kusahau

-Roho atakufundisha na kukumbusha jinsi ya kufanya usafi
na kuwa msafi

-Roho Mtakatifu atakufundisha jinsi ya kuongea mbele ya watu jinsi ya kubehave

-Roho Mtakatifu atakufundisha hata mambo ya chumbani kwa wanandoa.

-Roho Mtakatifu anakuonyesha out of you atakuonyesha watu wanakuchukuliaje ili ujirekebishe

-Roho Mtakatifu atakufundisha kufanya kazi, kufanya biashara,huduma

-Roho Mtakatifu atakufundisha jinsi ya kupanga ratiba

-Roho Mtakatifu atakufundisha kuvaa kupendeza

-Roho Mtakatifu atakufundisha kuwa wewe (original)

-Roho Mtakatifu atakufundisha kuchagua marafiki

-Roho Mtakatifu atakufundisha mambo yote ambayo huyawezi na utayaweza

-Roho Mtakatifu atakufundisha ku plan

-Roho Mtakatifu atakufundisha jinsi ya kuheshimu watu

-Roho Mtakatifu atakufundisha jins ya kujishusha

-Roho Mtakatifu atakufundisha jinsi ya kutokuwa bored

-Roho Mtakatifu  atakufundisha ujasiri

-Roho atakufundisha jinsi ya kuongea na mtu akukubali

-Roho Mtakatifu atakufundisha jinsi ya kukaa na boss mkorofi

-Roho Mtakatifu atakufundia hata jinsi ya kutembea

-Roho Mtakatifu atakufundisha hata jinsi ya kupika

-Roho Mtakatifu atakufundisha jinsi ya kushinda au wap pa kuanzia mradi wako

Roho Mtakatifu anafundisha KILA KITU ni wewe tuu. Bwana Yesu asifiwe.

Kuanzia mambo makubwa sana na madogo sana. Ya siri na yasiyo ya siri. Ya Rohoni na ya

mwilini. Kusudi ufanikiwe inakupaswa uombe akufundishe. Shida inakuja hapa tunatabia ya kumwaharakisha Roho

Mtakatifu hatumfuati kama Mungu

tunamfuata kama mjakazi. Uyu ni Mungu kabisa. Bwana Yesu asifiwe.lazima umfuate kama Mungu.

4.  Mwongozaji

Zaburi 32:8

. Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.

Kukufundisha ni jambo moja. Mtu anaweza kukufundisha bado ukawa huna

ujasiri wa kuanza. Bwana Yesu asifiwe. Roho Mtakatifu hatakufundisha tuu no!

Bali atakuongoza hapo anasema nitakuonyesha njia utakayoiendea manake atakutangulia atakushika mkono Bwana Yesu asifiwe

sana. Kumkosa Roho

Mtakatifu ni kukosa kitu kikubwa sana maishani mwako. Mwongozaji pia njiani katika safari anaendelea kukushauri kuhusu safari yako. Sioni jinsi Mkristo

anaweza ishi bila Roho

Mtakatifu sijui anapata wap iyo nguvu ya kushinda vita bila uyu Bwana mkubwa. Bila uyu Bwana mkubwa utakwama katika kila kitu unachokifanya Bwana Yesu asifiwe sana.

5. Mlinzi

Zaburi 32:8

.Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.

Hapo anaposema jicho langu litakutizama manake nini nitakuangalia ili usije jiingiza katika makosa. Watu

walikosea kufanya maamuzi. Walikosea kufanya maamuzi katika kuchagua

-mahali pa kuishi/alipopangisha

-eneo la biashara alipo

-mtu wa kuolewa/au kumuoa

-course ya kuchukua chuo

-kazi anayofanya

-marafiki

-maamuzi ya kununua vitu

-Biashara ya kufanya

-Shule aliyompeleka mtoto/watoto

-mahali alipojenga nyumba

- ramani ya nyumba iliyojengea nyumba

-Maamuzi kuhusu pesa

Kuna maamuzi mengi sana

binadamu tuliyafanya na ndio yametufikisha hapa tulipo. Kazi ya Roho Mtakatifu ni kukulinda ili usifanye maamuzi mabaya

Ili usije kujutia baadae maana gharama ya kufix kitu na Mungu ni gharama

kubwa. Hasa ambako kitu ambacho hukumshirikisha Mungu. Au ulijua wrong 

ukachagua Kuendelea anyway. Bwana Yesu asifiwe. Katika section ambayo inagharimu watu ni decision. Ndo mana Roho Mtakatifu

ameshuka ili yeye afanye

decision kwa niaba yako ili usije pata hasara. Bwana Yesu asifiwe sana.

 6. Kutupasha habari kwa habari ya haki,hukumu na dhambi

Unaweza kuokoka na bado ukaishi katika utumwa. Utumwa wenyewe ni upi ni kuishi katika sheria. Unakuta mtu tokea asubuhi anajichunga asifanye dhambi.

Anajichunga afanye haki, anajichunga asihukumu vibaya.

Bwana Yesu asifiwe! Anasahau tunaishi katika neema. Sasa ukiwa na Roho Mtakatifu ukienda wrong

kwa habari ya hukumu haki na dhambi hapo hapo atakujulisha. Pili huna haja ya kujichunga yeye mwenyewe

atahakikisha huendi kufanya makosa mambo ambayo

hayampendezi Mungu. Utakuwa unasikia uzito wa kunywa pombe! Uzito wa kuzini! Uzito wa kufanya uasherati. Uzito wa kudanganya! Uzito wa kuiba! Uzito

wa Kusengenya. Uzito wa mizaha inayotoa uwepo wa Mungu. Bwana Yesu asifiwe sana. Kwa iyo kazi mojawapo Ya Roho Mtakatifu ni kuhakikisha ilo lango linakaa

sawasawa. Bwana Yesu asifiwe. Kuna watu

wanahangaika wanasema nataka niwe mtakatifu. Utakatifu unakuwa controlled na Roho Mtakatifu na sio

Na Mwili huu. Kazi mojawapo ya Roho Mtakatifu ni kukusaidia ili uweze kukaa sawasawa. Bwana Yesu

asifiwe.

Yohana 16:8

. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.

7. Mpashaji habari wa mambo yanayokuja

Yohana 16:13

. Lakini yeye atakapokuja, huyo

Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Kama unataka kujua

mambo yanayokuja kuhusu

-Mahali unapoabudu

-Familia yako

-mme,mke,watoto wako

-Ofisini kwako

-Serikalini

-Katika ulimwengu wa Roho

-Biashara,kazi unayofanya,huduma

-Mwaka husika

Au whats ever its simple

ukinyenyekea Roho Mtakatifu atakuambia mambo yatakayokuja. Alimradi tuu unauliza kwa nia nzuri ya ki Mungu si sababu zako au

interest zako. Roho Mtakatifu ni mwaminifu tena atakuambia hata

usiyouliza. Ukitaka kuyajua uliza utayajua. Kama unataka uambiwe na watu basi

ngoja wakuulizie kisha wakuambie. Bwana Yesu asifiwe sana. Jina la Bwana libarikiwe.

8. Anafumbua mafumbo ya Mungu

1 Korintho 2:10

. Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

Jambo lolote fumbo katika maisha yako lisikupe

shida mshirikishe Roho Mtakatifu mwombe Roho Mtakatifu akufungulie. Funga omba msihi Roho Mtakatifu

akufunulie atakufunulia. Fumbo ni pamoja na mambo usiyoyaelewa. Siri usiyoielewa. Jambo lenye

utata Roho Mtakatifu

anauweza wa Kutrace case iyo kukufunulia chanzo. Sehemu iliyopo na nini kinatakiwa kifanyike uyo ni Roho Mtakatifu.

9. Hutuweka katika kweli yote

Yohana 16:13

. Lakini yeye

atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Kukuweka katika kweli yote manake kukufungua macho kuhusu swala flani. Ukimwambie Mungu niweke katika kweli yote kwa maana nyingine Mungu afungue

macho yako na masikio yako ya Rohoni.ili uweze

kuona kwa iyo badala ya kuhisi watu, kudhania watu mwombe Roho Mtakatifu afunue kweli. Akupe ukweli

wenyewe. Jina la Bwana libarikiwe.

10. Mkamilishaji au mtendaji Mkuu/coordinator wa mambo ya

Rohoni kuja mwilini.

Mwanzo 1:2

. Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Mwanzo 1:3

. Mungu akasema, Iwe

nuru; ikawa nuru.

*Roho ikawa juu ya maji akasema iwe nuru Roho akafyatua nuru. Hii manake yake nini? Manake ni hii Roho Mtakatifu ni msababishaji wa vitu.au producer wa

vitu Kama ni msababishaji

wa vitu  au mzalishaji wa vitu na wewe unahitaji ivyo vitu basi ujue kabisa bila yeye huwezi vipata. Kabla hata ya kumjua amekua

akikutengenezea na vingine unavyo je si zaidi ukawa karibu naye?

Utakuwa mshindi kila kona ya maisha yako. Bwana Yesu asifiwe sana. Roho Mtakatifu tuna

Mwitaji kuanzia utosi hadi uwayo. Tena katika kila kona ya maisha yetu na si sehemu ya ibada tuu. Bwana Yesu

asifiwe

Ni Muhimu kuliko hata Roho yako.

NINAMPOKEAJE ROHO MTAKATIFU....

Bwana Yesu asifiwe!

Zipo njia tatu za kumpokea Roho Mtakatifu

1. Kuwa na kiu na Roho Mtakatifu kumkaribisha aingie ndani

yako.njia wewe kuomba.

-mfano mimi nilijazwa na Roho Mtakatifu chumbani kwangu! Nilikuwa na kiu  nilimuomba Mungu anijaze Roho wake

Mtakatifu aniwezesha niseme kwa lugha mpya. Nilikiri sala ya toba

chumbani na kujazwa Roho Mtakatifu chumbani.

Luka 3:21

. Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka;

*ONA HAPO NAYE ALIOMBA! ROHO MTAKATIFU

ANAWEZA KUJA KWAKO KWA KUOMBA AJE KWAKO NA AKUJAZE.

Hii mara nyingi ni Mungu huwa anasukuma watu au mtu. Kunakuwa na automatic ndani yako ya kiu unajikuta

umeomba mwenyewe na umejazwa.

Ukiona

msukumo huu ndani yako basi jua Ni Mungu.Wengine walijazwa bafuni. Wengine jikoni. Wengine wakitembea. Wengine usingizi. Wengine wakisifu na kuabudu.

2. Neno linapofundishwa

Matendo ya Mitume 10:44

.Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno.

Matendo ya Mitume 10:45

. Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na

Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu.

Matendo ya Mitume 10:46

. Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,

Matendo ya

Mitume 10:47

. Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?

Kama hivi kwa kusoma habari za Roho Mtakatifu anaweza kuja juu yako kukujaza na

ukanena kwa lugha mpya. Neno

Likimgonga Sana mtu moyo unafunguka Roho Mtakatifu ataangalia ile kiu iliyopo ndani basi kama moyo umefunguka anakujaza.Bwana Yesu asifiwe Sana.

3.Kuwekewa mikono na Mtu

aliyojazwa Roho Mtakatifu

Matendo ya Mitume 19:1

. Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko;

Matendo ya

Mitume 19:2

. akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia.

Matendo ya Mitume 19:3

. Akawauliza, Basi mlibatizwa kwa

ubatizo gani? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana.

Matendo ya Mitume 19:4

. Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu.

Matendo ya Mitume 19:5

. Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la Bwana Yesu.

Matendo ya Mitume 19:6

. Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza

kunena kwa lugha, na kutabiri.

Ingawa ni muhimu Sana kuwa na hakika ni nani anakuwekea mikono. Ikibidi funga kwanza omba umjue uyo Mtumishi. Usitishwe na ishara maajabu

yanayofanyika Mungu alisema

muichunguze kila Roho. Msikubaliane Na kila Roho. Soma maandiko funga. Mwombe Mungu akufunulie kuhusu uyo Mtumishi kabla ya kupeleka kichwa chako

kuwekewa mikono mikono mingine inamuunganiko wa

kipepo akikuwekea tuu mikono tayari anaku connect na kuzimu. Bwana Yesu asifiwe. Sasa Mtu

Aliyejazwa Roho Mtakatifu akikuwekea mikono akiomba wewe ujazwe Kuna kuwa na Impartation ya Roho Mtakatifu

gafla na  wewe utaanza nena kwa lugha mpya. Bwana Yesu asifiwe.

*KITU MUHIMU KATIKA YOTE KATIKA HAYO MATATU HAKIKISHA UMETUBU. KAMA HUJATUBU NA UNANENA KWA LUGHA BASI JUA YA KWAMBA HIYO SIO

LUGHA YA ROHO MTAKATIFU. SAA INGINE UNAWEZA NENA KWA LUGHA UKAFIKIRI UNANENA KWA LUGHA KUMBE UNANENA KWA LUGHA YA MAPEPO.

HIVYO NI MUHIMU SANA KUSOMA NENO! KUSIFU KUABUDU KUTUBU KISHA NDIPO UNENE KWA

LUGHA. KITU KINGINE

CHA MSINGI UKIJAZWA MARA MOJA IMETOSHA YAKUPASWA UENDELEE KUNENA UNAPOZIDI KUNENA ILE LUGHA INAENDELEA KUBADILISHWA. NA KUWA YA KWAKO.

Swali nitajuaje kama Roho Mtakatifu yupo ndani

yangu au nitajuaje ninaye?

Jibu it's simple

Utaangalia vile vitu ambavyo Roho Mtakatifu anavyo kama na wewe unavyo yani tabia za Roho Mtakatifu au Matunda ya Roho Mtakatifu kukaa ndani ya Mtu.

Ukiwa na Roho Mtakatifu utajua si swala la kuhisi. Mabadiliko utayaona ndani mwako Kwa kiasi kikubwa kuanzia ndani mpaka nje. Maneno yako yatakuwa

ushuhuda wa Kristo. Matendo yako yatakuwa ushuhuda wa

Kristo, mawazo yako yatakuwa ushuhuda wa Kristo. Bwana Yesu asifiwe Sana.

Wagalatia 5:18

. Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

Wagalatia 5:19

. Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo

haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

Wagalatia 5:20

. ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

Wagalatia 5:21

. husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na

hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

ROHO MTAKATIFU AKIINGIA NDANI YAKO HAYO MATENDO HAPO JUU

HAMU YAKE INAKATWA INAKUWA DISCONNECTED.

HAITAKUWA MARA MOJA BUT KIDOGO KIDOGO MWISHOWE INATOKEA ILE HALI YA KUCHUKIA HAYA MATENDO NA YANAYOFANANA NA HAYO.

Wagalatia 5:22

. Lakini tunda la Roho ni

upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

Wagalatia 5:23

. upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.

HAYO HAPO JUU NI MIFANO MICHACHE YA MATUNDA YA ROHO MTAKATIFU.

IVYO UNAWEZA TUMIA IYO KAMA TESTER.  INGAWA ROHO MTAKATIFU

AKIWA NDANI YAKO HUNA HAJA YA KUAMBIWA NA MTU WA NJE ATAKUSHUHUDIA NDANI YAKO NA UTAJUA KABISA UNAYE ROHO MTAKATIFU.

JINA LAKE MUNGU LIBARIKIWE!

  *kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu

josephntandu@gmail.com,0713297066/0765377506

Comments

Popular posts from this blog

MAOMBI HATARI YA KUVUNJA UCHAWI WA MAFUNDO

MAOMBI YA KUFUNGUA KIBALI CHA  NAFASI YA KAZI

MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA KUCHELEWESHA