ARDHI IMEBEBA ROBO TATU YA MAISHA YA BINADAMU



Bwana Yesu asifiwe. nimrudishie Mungu utukufu kwa neno lake. naomba Mungu akupatie kitu cha kukusaidia unapoanza kufuatilia somo hili. Na akupe ujasiri wa kufanya yakupasayo!

Somo: "Ardhi imebeba robo tatu ya maisha ya binadamu"

Kwanini ardhi? Na sio maji? Au Anga?

Mwanzo 12

1 Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2  nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;

3  nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.

4  Basi Abramu akaenda, kama Bwana alivyomwamuru; Lutu akaenda pamoja naye. Naye Abramu alikuwa mtu wa miaka sabini na mitano alipotoka Harani.

*pigia mstari neno HARANI. nitaja kukuonyesha huko mbele.

*Mungu akikuita ni lazima atakuahidi kitu. Amekuita uokoke jua kuna kitu atakupa. Amekuita kwenye huduma yoyote jua kuna kitu Mungu atakupa. Mungu ni Mungu wa mipango na maagano ya kweli si umeona hapo juu Mungu aliingia mkataba na Abramu, ndipo Abramu akakubali kutoka nyumbani mwa Baba yake.

Tuendelee....

7  Bwana akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu Bwana aliyemtokea.

8  Kisha akaondoka huko akaenda mpaka mlima ulio upande wa mashariki wa Betheli, akaipiga hema yake; alikuwa na Betheli upande wa magharibi, na Ai upande wa mashariki, akamjengea Bwana madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana.

 9  Naye Abramu akasafiri, akazidi kwenda pande za kusini.

*Abramu alimjengea Mungu madhabahu. Alijenga wapi? juu ya ardhi.

Tuendelee....

Mwanzo 28-10-13

10  Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani.

 11  Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.

 12  Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.

 13  Na tazama, Bwana amesimama juu yake, akasema, Mimi ni Bwana, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako.

*Yakobo mjukuu wa Abramu naye akaenda HARANI sehemu ile ile Babu yake aliyoijenga madhabahu!

*kilichomtoa Yakobo mpaka Harani mimi na wewe hatujui. Lakini cha kushangaza ikawaje Yakobo akaenda kulala sehemu ileile Babu yake aliyomjengea Mungu Madhabahu. Wakati huu Mungu bado hajajitambulisha kama ni Mungu wa Yakobo. Bado alikuwa anaitwa Mungu wa Abramu.


*Alivyolala Yakobo aliota ndoto, kazi imetoka pale alipolala kuelekea mbinguni. Tena malaika wanapanda na kushuka.

*Ilikuwa imepita zaidi ya miaka ishirini kumbuka

*Mungu akamtokea Yakobo katika ile madhabau, Mungu akaahidi katika ile madhabau.

*Nataka nikufundishe kitu ulimwengu wa roho wowote haufanyi kazi bila madhabahu. Uwe ulimwengu wa ibilisi au wa Mungu Yehova lazima kuwe na madhabau ya kuwapa nguvu au maagizo hao watumishi wa iyo madhabau.

*unauliza nimejuaje? Jiulize kwanini Mungu asiongee kote au asiahidi kote ni mpaka kwenye ile madhabahu. Na madhabau ile ilijengwa katika ardhi. sababu binadamu yoyote mambo yote yalianzia kwenye ardhi.

Hata mwili wako ni udongo. Vitu vyote juu ya ardhi vyote vimejengwa na ardhi. Kwa iyo ardhi ni mbegu ya Mungu. Mwingine atauliza ardhi ilitokea wap? Ardhi ni pumzi

 ya Mungu. Iyo pumzi moja tuu ya Mungu ndiyo iliyotengeneza kila kitu. Juu ya ardhi, simu unayoisoma, makaratasi, pesa, nyumba unayoishi kila kitu juu ya ardhi kilitokana na udongo. Bwana Yesu asifiwe sana.

Tuendelee...

Mwanzo 28-16-19

16  Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua.

 17  Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni.

18  Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake.

 19  Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu

*Yakobo akasema BILA SHAKA HAPA NI NYUMBA YA MUNGU,NAPO NDIPO LANGO LA MBINGUNI

*tutafakari neno hilo hapo sehemu hii pangekuwa kuna madhabahu ya ibilisi je ingekuwaje? Yakobo pengine angeota

 anakimbizwa na wanyama, nyoka,au ndoto zozote zile za kutisha. na angeona ngazi imeanzia juu ya ardhi kushuka kuzimu. Kushuka chini ndiko kuzimu. Lakini ameota malaika wanapanda ngazi na kushuka kuelekea mbinguni.

*ardhi nyingi tunazoishi zina madhabau ya ibilisi. Labla si wewe uliyeweka lakini aliyekuuzia na aliyemuuzia aliwahi kuweka madhabau za ibilisi.

 Angalia mda ambao Abram alijenga madhabahu mpaka Yakobo alipoenda palepale. Ivyo madhabahu haina mda.

 Inaweza ishi milele. Ndo mana nyumba nyingi hazina utulivu. Ndio maana mwana wa Mungu ukienda kukaa sehemu yenye madhabau ya ibilisi lazima upate vita. 

Tuingie ndani kidogo....

Nia ya Mungu ni nini?

ISAYA 32:18

18  Na watu wangu watakaa katika kao la amani; na katika maskani zilizo salama, na katika mahali pa kupumzikia penye utulivu.

*masakani manake ni mahali unapoishi, Mungu kasema watu wangu watakaa kwa amani na kupumzika penye utulivu.

*Ilo neno linazungumzia ardhi ile yenye madhabau ya Mungu. Ardhi ambayo ina madhabau ya ibilisi huwezi kuwa kuna utulivu, hakuishi magonjwa, hakuishi ugomvi, hakuna amani. Watu wanaoishi

 nyumba iyo mapito hayaishi. Ni vita baada  ya vita baada ya vita. Unaweza kuta familia nzima inaisha kwa pressure au cancer au kuumwa kichwa watu wanakufa hawajui kumbe ardhi waliyokalia kuna ngome alifukiwa mzima,

 kuna jogoo alifukiwa mzima wakishafanya ivyo manake wamemkaribisha pepo au wamefungua mlango wa kuzimu. Na iyo tayari ni madhabau, kuna mbuzi mzima alifukiwa,

 kuna kondoo mzima alifukiwa kitendo cha kufukia tuu tayari pepo linakuja linakaa kwenye iyo ardhi, panakuwa madhabau na watu sasa wanatii sheria za yule pepo bila kujijua.

Mahali popote penye madhabau ya ibilisi juu yake lazima ilo  anga  aje mkuu wa giza ili kucontrol hao watu. Ndo anawasukuma kufanya matambiko. Kumwaga damu. Watu wanakuwa

 controlled kupitia iyo madhabau, kwa iyo madhabau sasa ndo inayowapa wachawi, waganga wa kienyeji nguvu ya kutawala ilo eneo nguvu.kwa iyo unaweza kukuta mtaa mzima kuna nyumba moja tuu ipo madhabau ya ibilisi!

Serikali yote ya ibilisi ya huo mtaa lazima waende hapo kupewa maelekezo au kupewa nguvu. Sasa wewe mpendwa  hujui A wala B umeenda kukodisha, au kupanga au kukaa,kununua tayari ile madhabau inaanza kukupiga vita.haufanikiwi katika lolote. Kwa kuwapa wale margent wa kuzimu nguvu za kukushambulia.

Tuingie ndani zaidi....

Ufunuo 2-12-13

12  Na kwa malaika wa kanisa lililoko Pergamo andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na huo upanga mkali, wenye makali kuwili.

 13  Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani; nawe walishika sana jina langu, wala hukuikana imani yangu, hata katika siku za Antipa shahidi wangu, mwaminifu wangu, aliyeuawa kati yenu, hapo akaapo Shetani.

*Nataka nikupe siri ili uone utamu wa biblia kitabu cha ufunuo ni majibu ya makanisa yale saba (7) ya Kristo! Ndio maana unasikia anasema na malaika wa Pergamo andika, malaika wa Efeso, Filipi haya ni makanisa Yesu alikuwa anajibu

 majibu yao, Yesu alikuwa anawaita malaika anawambia andika uwapelekee majibu hayo. Ndio maana anasema andika anawapa majibu hayo ili wawapelekee makanisa hayo ndio maana anasema andika!

Anasema napajua ukaapo ndipo penye kiti cha enzi cha shetani! Anasema najua umeshika sana jina langu, hukuikana imani yangu, hata Antipa shahidi yangu, aliyeuwawa kati yenu akaapo shetani. Yesu alikuwa anawaambia kuwa hapo

 mnapokaa kuna kiti cha enzi cha shetani, kuna madhabau ya shetani! Ilo ndilo tatizo. Yani manake iyo ardhi mnapoishi kuna madhabahu ya shetani. Kwa iyo ili kanisa lilikuwa linapata vita alafu alijui vita inatoka wapi,

 sasa ndo wanamuuliza Yesu maswali magumu hawaelewi. Ni kama wewe jinsi ulivyokazana na wokovu lakini bado unapata vita.... Haviishi. Haya majibu yametolewa mpaka kwenye kanisa la leo, watu hawasomi biblia tatizo. Bwana Yesu Asifiwe.....


Tuingie ndani sana sasa.....

Ufunuo 13-1-2

1 Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.

2  Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.

*Wote tunafahamu fahamu stori hii uyu alikuwa ni mnyama wa ajabu aliyotoka chini ya bahari. Ni mnyama ambaye Ibilisi akampa nguvu zake na kiti cha enzi na uwezo mwingi.

Ndio maana kuna sehemu unaweza ukalala ukaota unakimbizwa na wanyama mara dubu, simba, chui jua kwamba hapo ulipolala kuna viti vya enzi vya ibilisi. Sasa nikupe siri ingine hivi vitu haviji kama kuja tuu.

Wakitaka kuweka kiti cha enzi cha shetani watazika kitu kizima, na kwa manuizo ya maneno ya maagano. Si kila kaburi ni kaburi makaburi mengine ni madhabahu!

 Kabla ya kuzika mtu pengine walitanguliza mbuzi mzima au kuku mzima. Mizimu ni watu waliokufa. Wanawasiliana nao kwa kupitia mapepo. Mambo haya yanatisha lakini lazima tuyaongee ili ujue uzito wa ardhi, ardhi ya namna hii au ukoo wa namna hii wewe mtakatifu wa Mungu ni lazima upigwe vita. Joka atampa yule mnyama nguvu ya kukupiga vita. Kukufanyia makufuru.

*Mstari 1 anasema mwenye makufuru mengi, ndio maana ukoo wowote au familia yoyote mtu akiokoka tuu wanamtenga unafikiri ni kwa nini?si wao! Hata kama hawamwambii lakini kuna mipaka flani utaiona tuu baina yako wewe

 na wao. Ni sababu ya uyu mnyama wa ibilisi. Unaweza ukaokoka na ukapigwa vita na kila mtu! Kumbuka anayekupiga vita ni ibilisi maana kwa wewe kuokoka manake utaweza kuzuia madhabahu kwa upande wa Baba yako zisifanye kazi. Kwa upande wa Mama yako zisifanye kazi.

Hapa ndipo unaposhangaa vita haziishi, ndipo wapendwa huwa wanapata shida hasa tena wewe ndio wa kwanza kuokoka.
 Kwa iyo ile madhabahu ya uyu mnyama inatengeneza chuki na watu waliokuzunguka hata ndugu zako au Baba yako ili wakupige vita.utaona tuu kwa matendo hata kama hawasemi. Na kuna baadhi ya vitu hutashirikishwa.


 Ibilisi anawawekea hasira ili wakumalize. Kinacholindwa ni wewe usije gusa ile madhabahu maana ukigusa tuu umeharibu ndo mana unapata vita katika kila kitu. Hawana nguvu tena.

Kuna shuhuda moja; dada mmoja toka mwanza alikuwa mwislamu mbegu ya Kristo ikamdondokea moyoni mwake si unajua kunatofauti ya kuokoka kwa kuombewa (kusukumwa kwa maombi) na mbegu ikidondoka moyoni sasa uyu dada aliyekuwa kwao mwislamu kabisa.

 mbegu ya Kristo ilidondoka, akawa anaenda kuomba na baibui lake kanisani. Sasa Baba yake ambaye ni mkubwa wa mizimu kuna namna wale mapepo walimjulisha maana mambo yao yalikuwa hayaendi tena,

basi wakamchunguza kupitia shangazi yake wakamkanya yule Dada. Yule Baba akamwambia mtoto wake ukienda tena kusali huko wewe si mtoto wangu tena. Kama unavyojua mbegu ya Kristo ikikudondokea  huwezi jizuia akaenda

 tena. Yule mzee alijua maana kila akienda ile madhabahu ya yule mzee haifanyi kazi. Akakasirika akachukua bunduki akaikoki ile anataka kufyatua yule dada akasema kuna mwanga mweupe ukaja mbele ya ile bunduki kwenye lile tundu la kutolea risasi, akifyatua haitoki.

Akilenga juu inatoka. Kwa iyo ndo ikawa pona yake. Sasa jiulize kwanini mtu aombe tuu mwingine atake kumuuwa? Jua hili limnyama linauwezo wa kumbebesha mtu hasira au watu hasira wakawa adui zako.

Na utashangaa ukibomoa tuu iyo madhabahu  ya uyu mnyama watu haohao waliotaka kukuuwa wanakuwa tena upande wako. Madhabahu kwenye katika ardhi ni kitu kina nguvu sana.

*Shetani huzipa nguvu madhabahu zake ili kufanya vita na watakatifu.pamoja na wewe

*ukiona unaenda sehemu unapata vita unaenda sehemu ingine hupati vita jua hapo unapopata vita chini kuna madhabahu ya ibilisi.

*ukiona vita haviishi, vinajirudia kila mara au tatizo linamwendelezo jua katika iyo ardhi unayokaa kuna madhabau ya ibilisi

*90% ardhi ya Tanzania ardhi yake haiko salama kuna madhabau za ibilisi. Vitu vingi sana vimezikwa  katika ardhi ya Tanzania. Mtumishi mmoja aliwahi toka Kenya kuelekea Tanzania alipofika mpakani akawa anagawa vikaratasi vya ujumbe wa neno la Mungu,

 anasema alipokuwa anagawa Tanzania walikuwa wanamtukana matusi ya nguoni kabisa. Alipokuwa akienda upande wa kenya akigawa watu walikuwa wanamshukuru na kumbariki.

 Mungu akamwambia ardhi ya Tanzania si salama kama ya Kenya. Sehemu nyingi ni malango ya ibilisi. Ndo mana alikuwa anatukanwa kilichokuwa kinamtukana si wale watu  ni yule

 mnyama kupitia madhabahu ambazo sisi watanzania tumezijenga toka enzi na enzi. Anga letu bado halijafunguka kama la Kenya.

* Kufanikiwa kwa mtu inategemea na mahali anapokaa. Kwa iyo vita nyingi wanayopata wapendwa 100% inatokana na ardhi ya kwenu, kwa Baba yako, kwa mama yako. Ulipopanga, uliponunua. Kama kuna madhabahu za giza hizo ndizo zinakupiga vita.

Unachokiona wewe katika maisha yako ni matokea ya vita za izo madhabahu. Ndo mana unaweza lala nyumba moja chumba hiki ukalala kwa raha. Chumba hiki kingine ukaota ndoto mbaya. Unakimbizwa na simba au kuna mnyama hata

 asiyeeleweka anayetisha.Sasa kufanya vita na matokeo huwa hakumalizi tatizo. Ni mpaka ardhi iponywe. Ni mpaka iyo madhabahu kupitia iyo ardhi ivunjwe. Vitu vya enzi vibomolewe. Kuna mambo utayaombea utavuka lakini Kuna vitu vingine vimefungwa kupitia ardhi.

 Inapovunjwa basi wafalme wa giza wanakosa nguvu, wachawi wanakosa nguvu maana hakuna kitu kinachofanya kazi bila madhabahu. Ndo mana mtu anaombewa anawekewa  mikono na Mtumishi mwenye annoiting kubwa lakini baada ya mda vita vinaibuka tena.

 Ukiona ivyo ujue ni vita vya madhabahu kupitia ardhi iliyounganika au unganishwa na wewe kwa njia moja au nyingine. Au jiulize kwanini ukiwa kanisani unasikia

 amani sana na hewa nyepesi hutamani hata kuondoka. Na kwanini ukirudi nyumbani husikii iyo amani ushawahi jiuliza? Jibu ni kwamba kanisani kumejengwa madhabahu ya Yesu na kwako hujajenga. Anga halijafunguka.

*Vita vya kiuchumi, ndoa, kutokupata watoto, kazi, umasikini, na yanayofanana na hayo inategemea sana na ardhi ya maisha yako ikoje.

 Ardhi inaponywa na kufunguliwa jinsi inavyofunguka ndivyo jinsi wewe unaanza kuona wepesi katika sehemu zilizokuwa zinakupa wakati mgumu. Ndo mana kuna maeneo ukienda utapata shida sana

 unaweza fikiri hakuna wokovu. Mfano mtu aliyewahi enda zanzibar au aliyewahi enda India kule utapata shida sana kuomba au kusoma neno. Arshi ya kule imeshikiliwa na viti  vya enzi vya ibilisi.


Jinsi ya kuomba sasa kibiblia ungana nami part B ambayo ndo muhimu kupita yote. Kuombea ardhi unapoishi, au ardhi ya kwenu. Na jinsi ya kuombea sehemu za kazi au biashara pia kuna maombi yake tofauti. Tutaelekezana. Jina la Bwana libarikiwe

kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu


josephntandu@gmail.com,0713297066

Comments

  1. Ubarikiwe mno nimelipenda somo la Kuombea Ardhi kwakweli nimefunguliwa mno, Ubarikiwe mno kwa ufafanuzi huu leo ninaamini nimekuwa mpya katika Jina la Yesu ardhi ninayokaa inaenda kutakaswa kwa Damu ya YESU🙏🏿

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

MAOMBI HATARI YA KUVUNJA UCHAWI WA MAFUNDO

MAOMBI YA KUFUNGUA KIBALI CHA  NAFASI YA KAZI

MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA KUCHELEWESHA