IMANI INAFANYA KAZI KWA KUTAMBUA MAMLAKA ILIYO KATIKA JINA LA YESU





Bwana Yesu asifiwe. 

Tupandishe imani zetu kwa neno hili na tafakari yake. Neno unalijua tuangalie lugha ya neno ya leo.Nimshukuru Mungu wa BWANA WETU YESU KRISTO.ni mda mwingine tena wa kujifunza neno la Mungu

Luka 7

2  Na mtumwa wake akida mmoja alikuwa hawezi, karibu na kufa; naye ni mtu aliyempenda sana.

3  Aliposikia habari za Yesu, alituma wazee wa Wayahudi kwake kumwomba aje amponye mtumwa wake.

4  Nao walipofika kwa Yesu, walimsihi sana wakisema, Amestahili huyu umtendee neno hili;

5  maana, analipenda taifa letu, naye alitujengea sinagogi.

6  Basi Yesu akaenda pamoja nao. Hata alipokuwa si mbali na nyumba yake, yule akida alituma rafiki kwake, akamwambia, Bwana, usijisumbue, maana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu;

7  kwa hiyo nilijiona sistahili mwenyewe kuja kwako; lakini, sema neno tu, na mtumwa wangu atapona.

8  Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.

 9  Yesu aliposikia hayo alimstaajabia, akaugeukia mkutano uliokuwa ukimfuata, akasema, Nawaambia, hata katika Israeli sijaona imani kubwa namna hii.

 10  Na wale waliotumwa waliporudi nyumbani, wakamkuta yule mtumwa ni mzima.

*Halleluyah halleluyah! Neno hili watu wengi wanalijua na wameshalisoma nachotaka kukuuliza kwanini akida alisema sema neno moja tuu. Tatizo si imani aliyokuwa nayo!

Tatizo Ni nini kilimsukuma kusema vile !?. Ukijua kilichomsukuma kusema ilo neno "sema neno moja tuu" ukikijua hicho kilichomsukuma basi imani yako itatoka sehemu moja kwenda sehemu ingine.

Imani si kusikia tuu Bali na kuamini, wengi kusikia tunasikia. Lakini hatuamini. Ile hakika ya mambo yatajariwayo huwa haikamiliki pamoja na kusikia neno. Imani

 huja kwa kusikia. Wengi tunasikia. Imani ni hakika ya mambo yatajariwayo! Hapo ndipo tunakwama. Umeamka huna hata 100 mfukoni. Kukiri kusema mpaka ifike saa 10 jioni nitakuwa na mil 1, mfukoni.

Ndani mwako ukisema ni kama Kuna Moto unakurudia! Siyo? Iyo inataka imani ya hakika . Hatuamini mambo yatarajiwayo sababu kutokujua au kutambua mamlaka ya jina la Yesu.

 Kupitia kusikia kwa neno. Ngoja niongee lugha rahisi. Ni hivi bila kutambua mamlaka ya jina la Yesu huwezi amini kinachotaka kutokea kutokea.

Angalia hapo juu kwenye ilo neno anapomuelezea Yesu mstari wa 8, Mimi nami ninamamlaka yangu nikimwambia uyu Nenda huenda. Uyu njoo naye anakuja.  Akida alitambua mamlaka ya

 Yesu,ndo mana akajifananisha yeye na Yesu kwa hapa duniani, Mamlaka iliyobebeshwa kwenye ardhi, katika anga na bahari na mbingu zote,soma waefeso  1-17-23.kilichofanya Yesu akasema sijaona imani kubwa namna hii ni hakika ya kutambua mamlaka

 na kuijua kuwa Yesu Hana limitation kuwa anaweza kufanya lolote.Yes! Iyo ndo ilimfanya Yesu amshangae! Ivyo hata tatizo lake haliitaji Yesu afike kwake! No! Sababu tayari hata kwenye sauti ya Yesu

 tuu akitamka lile tatizo linasikia haijalishi yupo au hayupo. Kuna mamlaka. Ndo mana huitaji kumuona Yesu unahitaji jina lake ulitumie kwa imani.Unajua kila kitu kinasikia sauti ya Mungu. Ndio maana watumishi

 wakisema pokea uponyaji lile neno linatoka na mamlaka Yesu yani nafasi katika kuponya linaenda kwenye ugonjwa. Ugonjwa ndio unaisikia lile neno  sio masikio ya kichwani. Ugonjwa una masikio,Biblia inasema Bwana hulituma neno lake, kuwaponya. Kinachomponya mtu wewe kusikia na masikio yako. No ni ile situation

 imesikia ile mamlaka ya jina la Yesu na siyo masikio yako ya binadamu. Kama ni masikio inakuwaje unasikia kwa masikio then unapona mgongo? Hili ni somo lingine tutaangalia another time. katika

 ulimwengu wa roho lile tatizo linasikia. Kinachofanya watu wengi wasiamini neno au wazoee neno, au neno walione ni kitu cha kawaida ni kutokutambua

 mamlaka ya Yesu kwa uzito.YANI HILI NENO LIMEBEBA  MAMLAKA KIASI GANI AU NAFASI KUMALIZA TATIZO LANGU?  SITUATION YANGU? yani nafsi ya ilo neno katika shida yako iyo ndo shida ya wengi katika imani , kumbuka mfano wa

 Bahresaa kule juu. Ni kama vile mtu akitaka kukusaidia utataka ujue uwezo wake kwanza, anafanya nini? Mfano Raisi akisema nitakusaidia utakuwa na hakika.sababu ya nafasi aliyonayo. Watu wasio na imani si kwamba

 hawasomi neno, si kwamba hawataki kuliamini neno hapana.si kwamba hawaombi hapana  Its simple huwezi kulipa tatizo lolote uzito Ni mpaka liwe na  uzito kwenye akili yako. Hujanielewa! Kwenye mioyo Yao Yao hakuna hakika

 kama mamlaka ya jina la Yesu itamtoa kwenye magumu,yani hawaamini ilo neno kweli Lina mamlaka ya kumaliza shida yake iyo ndo tatizo.jinsi anavyoamini ndio matokeo anayopata,majaribu anayopitia,

 hawana hakika ya mamlaka iyo isiyoonekana kama kweli itamsaidia kwenye tatizo lake.ingawa neno wamelisikia.  Ukisema Bahresaa, Ni tajiri unamwelezea mtu

 mwingine ule uzito unaojua wewe kwa mwingine hawezi amini. Chukulia Bahresaa humfahamu kabisa alafu

 anakuambia mtu kuhusu bahressa, utasikia lakini hutaamini kwa uzito ule jinsi yeye anavyomuamini ni mpaka pengine uanze kuona bidhaa zake kwa wingi masokoni, ukiona azam

 television,  ukiona magari ya bahressa yakienda mkoani. Ukiona miradi yake mikubwa ndipo Utaamini.Kwa iyo ukiwa na shida ya mil 10, ukaambiwa bahressa kaelezewa tatizo lako unatakiwa ukaonane naye, kesho saa tano! Je hutakuwa na hakika

 tatizo lako kuisha? Jibu ni ndiyo! Iyo hakika imetoka wap? Iyo hakika imetokana na wewe kuujua uwezo wa bahressa. Nafasi ya bahressa! Kama wengi tungeenda kwa

 Yesu kwa nafasi yake katika neno lake la ahadi! Au la agano kwa kuitambua hakika ya mamlaka ya Yesu, juu ya tatizo tulilonalo basi tungesogeza milima mikubwa mbele yetu.ukiwa unaitambua unaijua na

 unaikubali mamlaka ya Yesu juu ya ilo neno kwenye biblia! Na ilo tatizo lako basi mambo Mengi ungeyavuka. Na utapokea kila ahadi bila wasiwasi na itatokea kwako hata kama imekawia hutakuwa na mashaka.

IMANI =  kusikia neno+ kuwa na hakika ya mambo yatajiriwayo haina ya mambo yasiyoonekana + kuamini mamlaka inayoenda kutekeleza mambo yatajiriwayo.

Embu tuangalie watu waliokuwa na matatizo ya kuijua mamlaka, kuitambua na kuiamini.

Marko 9:23

23  Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.

 24  Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.

 25  Naye Yesu akiona ya kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi, mimi nakuamuru, mtoke huyu, wala usimwingie tena.

*wengi stori hii mnaijua. Huyu Baba haukuitambua nafasi ya Yesu ya Kimamlaka . Kule juu ndo mana alisema ukiweza unaweza nisaidia, akasema yote yawezekana kwake aaminiye. Ndo mana wanafunzi wa Yesu

 walishindwa kumtoa yule pepo kwa yule kijana. Tatizo halikuwa kwa wanafunzi wa Yesu tatizo lilikuwa kwenye imani aliyoibeba yule Baba mwenye mtoto. Alivyotambua ilo ndo mana akamwambia Yesu nisaidie kutokuamini kwangu.

Mathayo 8-23-27

23  Akapanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata.

 24  Kukawa msukosuko mkuu baharini, hata chombo kikafunikizwa na mawimbi; naye alikuwa amelala usingizi.

 25  Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia.

 26  Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu.

 27  Wale watu wakamaka wakisema, Huyu ni mtu wa namna gani hata pepo na bahari zamtii?

* hapa wanafunzi wa Yesu hawakutambua nafasi ya Yesu ya kimamlaka ndio maana walihangaika. Walivyoona wameshindwa ndipo

 akamwamsha, si unaijua hii stori ya mawimbi yaliyotikisa mtumbwi baharini na Yesu akiwa ndani yake? Yesu akawaambia mbona mmekuwa waoga wenye imani

 Haba? Manake nini kwanini hamkuniamsha mda wote huo! Hamkuniamini ni mpaka mmeshindwa. Kitabu cha Luka stori hii inaelezea jinsi ilivyokuwa walikuwa

 wakitoa maji kwenye mtumbwi kabisa. Fuatilia stori hapo juu. Ni mpaka walipotambua nafasi ya Yesu ya kimamlaka.katika mtumbwi. Ndio mana wakasema uyu ni mtu wa aina gani hata pepo zinamtii?

SASA TUANGALIE WATU WALIOKUWA WENYE IMANI NA WALITAMBUA MAMLAKA YA YESU. AU NAFASI YA YESU KATIKA KUWAPONYA


Marko 9-27-31

27  Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Mwana wa Daudi.

 28  Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili?
 Wakamwambia, Naam, Bwana.

 29  Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate.

 30  Macho yao yakafumbuka. Naye Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema,
 Angalieni hata mtu mmoja asijue.

 31  Lakini wakatoka, wakaeneza habari zake katika nchi ile yote.

*Nataka uone imani yenye hakika ya kutambua nafasi ya kimamlaka aliyonayo Yesu Katika kutatua tatizo Lao. Hao vipofu walikuwa hawaoni. Sembuse wewe unayeona na kusoma biblia na kuangalia

 shuhuda. Kutokuona manake Ni kutokujua njia ya jawabu ya tatizo lako. Wao walikuwa hawaoni kabisa macho ya damu na nyama. Kwa iyo imani Yao

 ilijengeka kwa kusikia baada ya kusikia mioyoni mwao wakatambua nafasi ya kimamlaka aliyonayo Yesu,ingawa hawaoni unauliza nimejuaje? Yesu

 aliwauliza mnaamini kuwa naweza kufanya hivi? Yani manake mnatambua kuwa ninayo mamlaka ya kuponya? Mnahakika mamlaka yangu yanaweza kuwaponya? Iyo ndo maana yake!

 Wakamwambia naamu Bwana. Sasa angalia! Wasingetambua Yesu asingewaponya!  Wasingeijua nafasi ya Yesu wasingeponywa. Na wasingeikubali nafasi ya Yesu pia wasingeponywa. Wengi

 leo hii aidha unaijua unaitambua lakini hatuikubali nafasi ya Yesu katika matatizo yetu. Hatukubali neno la Yesu katika kutusaidia. Kuijua ni kitu kingine, kuitambua ni swala lingine bali kuikubali.

 Kuikubali ndio connection yako wewe na Yesu. Manake unaweza soma neno alafu wewe mwenyewe umelielewa lakini akili yako haikubaliani kuwa ili neno kweli linaweza kungoa huu mlima. Na hii

 hutokea sababu ya wewe kulinganisha maneno. Badala ya kulinganisha mamlaka. Kinakujia cha kwanza ni ukubwa wa tatizo, ugumu wa tatizo, au historia ya tatizo. Kinachotakiwa cha kwanza ni

 uwezo wa mamlaka ya Yesu. Kisha neno la Yesu limesema nini. Baada ya kutambua sasa ndipo jina la Yesu litafanya kazi vizuri kwa imani Hili ndilo tatizo kubwa katika imani zetu siku hizi. Huwezi kukivalue kitu

 kama hujui thamani yake. Huwezi tambua uwezo wa jina la Yesu kama hujui mamlaka zake. Kama hujui nafasi ya

 mamlaka katika tatizo lako. Ukiwa unajua nafasi ya mamlaka katika tatizo lako. Au nafasi ya Yesu kupitia neno lake. Basi nakuambia utaangusha milima. Jina la Bwana libarikiwe.

kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu


josephntandu@gmail.com,0713297066


Comments

Popular posts from this blog

MAOMBI HATARI YA KUVUNJA UCHAWI WA MAFUNDO

MAOMBI YA KUFUNGUA KIBALI CHA  NAFASI YA KAZI

MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA KUCHELEWESHA