IMANI YA HAKIKA NI IPI?




Bwana Yese asifiwe wapendwa, Ninamshukuru Mungu Baba wa mbinguni kwa kutupa nafasi ingine tena ya kujifunga neno la imani, sifa na utukufu kwa Yesu pekee.
 "IMANI YA HAKIKA"

WAEBRANIA 1:11

1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

* embu leo tuangalie lugha tofauti ya  hili neno. Imani ni hakika. Hakika baina ya mambo yasiyoonekana. Yani hayapo.

Nikuulize swali unalala usiku kesho unapanga mipango yako. Kitendo hiko  manake ni hakika. Tena iyo hata waislamu wapagani wana iyo imani.

Ukisema ninaweza kuruka juu una miguu miwili. Una afya, iyo siyo imani inayoongelewa hapo juu. Bali Yule mtu asiyekuwa na miguu! Au hawezi

 kusimama akisema nina hakika nitaruka juu baada ya kuombewa ikatoka moyoni mwake basi iyo hakika basi ndiyo imani yake.

Ukisema nina hakika nitanunua gari na ela unayo iyo siyo imani inayoongelewa hapo juu. Maana ela unayo. Imani ni hii huna pesa kabisa. Au pesa haiwezi hata

 kununua baiskeli. Alafu inatoka moyoni unasema nina hakika kwa neno hili la Bwana nitanunua gari. Na ukaamini na kukubali moyoni mwako.

Ukiwa unafanya kazi kazini ukasema nina hakika mwezi huu nitapata mshahara iyo siyo imani inayoongelewa hapo. Maana kama una kazi ni kawaida utalipwa tuu.

 Imani ni hii mtu asiyekuwa na kazi kusema nina hakika mwezi unaokuja nitapata kazi nitapokea mshahara na nitatoa fungu la 10. Imani ni kuzungumza kitu ambacho huna hakipo. No

 possibilities. Ila unaongea sababu neno limesema na ukaamini lile neno. Imani ni hii kiwete anayetembea chini.miguu hainyooki kabisa. Kabla ya kwenda kwenye maombi anashona full sute ya mtu mzima na kusema nikitoka huko nakuja kuvaa

 na kutoka out kwa miguu yangu. Imani ni hii kipofu asiyeona kabisa kabla ya kwenda kwenye maombi atabeba biblia atasema baada ya kuombewa tuu nitasoma biblia yangu. Imani ni kuwa na

 hakika katika vitu ambavyo havipo. Wengi tunaweka imani katika mambo ambayo yapo kwenye uwezo wetu. Au ndugu zetu. Imani ni hakika ya mambo

 ambayo kwako hayawezekani na hayapo na unaona kabisa haiwezekani. Lakini iyo haiwezekani imebadilishwa uliposikia neno la Mungu na unaamini kwa mazingira ya

 nje haiwezekani ila kwa neno la Mungu tuu. Kuwa kwa hili neno Hakuna lisilowezekana. Imani ni kutokusikiliza ndani mwako kunasema nini au watu wanasema nini. Yani kama

 kupingana na dunia ionavyo! Watu walivyozoea! Au kawaida au utaratibu.au maneno ya watu. Imani ni kama uchizi flani! Wehu flani wa kiroho! Kuamini

 katika taratibu za dunia watu hawaamini. Kuona vitu ambavyo watu hawavioni. Kusikia vitu ambavyo watu hawawezi kusikia, imani ni kama kujitenga na msimamo wako bila kurudi nyuma. Ni

 kama kubaki mwenyewe tuu unayeona njia wakati wengine hawaoni njia Yani wewe unaenda tofauti. Ni kuamini kile kisichowezekana. Labla nikupe mfano huu!

Luka

30  Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

 31  Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

 32  Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.

 33  Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.

 34  Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?

 35  Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.

 36  Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa;

*Hapa tunaona jambo lisilowezekana kwa akili za Mariam! Lisilofikirika!hata angewaambia wengine wangembishia ni

 yeye na moyo wake! Offcourse aliguna moyoni, akifikiri akaona haiwezekani! Angalia maswali anayouliza? Litakuwaje jambo hili? Kitu nachotaka uone hapo malaika hakumwachia ni mpaka

 ameelewa asingeelewa na kukubali ile mimba isingeingia, ya roho mtakatifu. Angalia jinsi malaika anamuelezea! Tena tazama jamaa yako Elizabeth yule aliyetasa amechukua mimba tena ya

 uzeeni! Naye ana mimba ya miezi sita. Mariam akazidi kishangaa! Hee Elizebeth kachukua mimba? Akafikiria Elizabeth ni mzee alafu tasa alikuwa mzee wa miaka 80, akazidi kushanga sana.

 Akasema moyoni kama mwanamke mzee miaka 80 tena aliyechukua mimba na alikuwa tasa. Basi jambo hili unaloniambia basi pia kwangu litawezekana, imani kuwa na

 hakika na mambo ambayo katika akili, fahamu, macho masikio haviwezekani, hakika huwa haipigi hesabu itakuwaje kuwaje hii si kazi yako. Hesabu jinsi

 itakavyofanyika anayo Mungu. Nikuulize swala Musa alikuwa na hesabu ya kugawanya bahari ? Musa alikuwa na

 hakika. How? When? Siyo maswala yako, wewe unachotakiwa kuamini yasiyowezekana kwako lakini kwa neno linawezekana. Imani itafanya kazi baada ya kukubali!

 Ukishapata hakika niliyoongelea hapo juu. Basi lazima sasa ndani mwako itakuja kukubali yes! Inawezekana. Sio mdomoni no ndani kwako. Yani nafsi! Nafsi ndio adui mkubwa wa imani. Unachokisoma

 kwenye biblia nafsi inasema haiwezekani, inakuonyesha mazingira ya nje, au hali yako halisi ya sasa! Inakukumbusha ya zamani. Sasa dawa yake ni kuongea ulichokiamini. Kuijibisha nafsi! Kwa neno

 la Mungu. Ikisema angalia hali yako ya sasa! Ikikukumbusha ya nyuma! Ikitumia macho yako! Au mazingira uliyopo iongeleshe nafsi yako kwa neno itasikia. Sema ni kweli lakini neno la Mungu linasema hivi. In long run, au baada ya mda mfupi nafsi yako itanyamaza kimya  itakaa kimya baada ya kukaa kimya. Sasa

 ile hakika yasiyowezekana. Itakuwa juu. Hakika ikishakua juu moyo utakubali. Katika kiwango hiki sasa lolote mdomo utakao tamka kwa jina la Yesu inakuwa

 ivyo. Hata baada kutamka kuendelea kukiri ulichotamka no matter what situation. Haijalishi mazingira yataendelea kukuzonga. Kutamka mpaka umepata kile ulichokikiri. Kumbuka baada ya kukiri tuu

 kutakuja mawazo, maneno ndani yako. Au watu wa nje au mazingira ya kukupinga kile unachokiamini. Sasa what it matters ni kile unachokiri kukimaintain kwa mda

 wote. Kama umekiri cha shetani malaika wa shetani anafanyia kazi hapohapo. Kama umekiri cha Mungu malaika wa Mungu anafanyia kazi hapohapo. Iyo ndio siri ya imani. Bwana Yesu asifiwe sana.

kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu


josephntandu@gmail.com,0713297066


Comments

Popular posts from this blog

MAOMBI HATARI YA KUVUNJA UCHAWI WA MAFUNDO

MAOMBI YA KUFUNGUA KIBALI CHA  NAFASI YA KAZI

MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA KUCHELEWESHA