KWANINI NI MUHIMU KUAMBATANISHA NA KUJIUNGANISHA NA SADAKA YA YESU KWA NJIA YA SADAKA?
Somo fupi:
Umuhimu wa kuambatanisha na kujiunganisha maombi yako na sadaka kwa Yesu Kristo.
Wote
mnakubali Yesu ni sadaka kwetu. Yeye alifanyika sadaka kwa Mungu kwa ajili yetu
na sisi tukakubalika mbele za Mungu. Sasa kwanini unaunganisha maombi yako na
sadaka? Tunaunganisha maombi yetu na sadaka kwa sababu tunataka kujiunganisha
na sadaka ya Yesu. Sadaka inayotambulika mbele za Mungu ni ile ya Yesu. Ivyo
kwa wewe kutoa sadaka mbele za Mungu ni kitendo cha wewe kujiunganisha na damu
ya Yesu, kujiunganisha na madhabahu ya
Yesu. Kwanini tunafanya hivyo, tunafanya hivyo sababu sadaka pekee inayokubalika
mbele za Mungu ni ya Yesu Kristo. Kwa iyo sadaka zote lazima zipitie katika
mikono ya Yesu ndipo ziende kwa Mungu Baba. Haki yetu sisi tunaipata kupitia
Yesu. Bila Yesu hatuna haki. Bwana Yesu asifiwe sana!
Tuangalie
neno; fuatilia taratibu ni stori nzuri
ya kufundisha sana. Soma mpaka mwisho.
Hesabu 23
2 Na Balaki mwana wa Sipori akaona mambo yote
ambayo Israeli wamewatendea Waamori.
3 Moabu akawaogopa hao watu sana, kwa kuwa
walikuwa wengi; Moabu akafadhaika kwa sababu ya wana wa Israeli.
4 Moabu akawaambia wazee wa Midiani, Sasa jeshi
hili la watu litaramba vitu vyote vinavyotuzunguka, kama vile ng'ombe arambavyo
majani ya mashamba. Na Balaki, mwana wa Sipori, alikuwa mfalme wa Moabu zamani
zile.
5 Basi akatuma wajumbe kwa Balaamu mwana wa
Beori, hata Pethori, ulio kando ya Mto, mpaka nchi ya wana wa watu wake, kwenda
kumwita, akisema, Tazama, kuna watu waliotoka Misri; tazama, wanaufunika uso wa
nchi, tena wanakaa kunikabili mimi.
6 Basi, njoo wewe, nakusihi unilaanie watu
hawa; maana wana nguvu kunishinda mimi. Labda nitawaweza, tupate kuwapiga,
niwafukuze watoke katika nchi yangu, kwa maana najua ya kuwa yeye umbarikiye
hubarikiwa, na yeye umlaaniye hulaaniwa.
7 Wazee wa Moabu, na wazee wa Midiani,
wakaenda, wakichukua ujira wa uganga mikononi mwao; wakamfikilia Balaamu,
wakamwambia maneno ya Balaki.
12 Mungu akamwambia Balaamu, Usiende pamoja nao;
wala usiwalaani watu hawa, maana wamebarikiwa.
22 Hasira ya Mungu ikawaka kwa sababu alikwenda;
malaika wa Bwana akajiweka njiani, ili kumpinga. Basi alikuwa amepanda punda
wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye.
23 Na
yule punda akamwona malaika wa Bwana amesimama njiani, na upanga wake mkononi
mwake amekwisha kuufuta; punda akageuka upande ili kuiacha njia, akaingia
shambani. Balaamu akampiga punda ili kumrejeza njiani.
24
Kisha malaika wa Bwana akasimama mahali penye bonde, katikati ya
mashamba ya mizabibu, tena penye kitalu upande huu na kitalu upande huu.
25 Yule
punda akamwona malaika wa Bwana, akajisonga ukutani, akamseta Balaamu mguu
wake, basi akampiga mara ya pili.
26
Malaika wa Bwana akaendelea mbele akasimama mahali pembamba sana,
hapakuwa na nafasi ya kugeukia mkono wa kuume, wala mkono wa kushoto.
27 Yule
punda akamwona malaika wa Bwana, akajilaza chini ya Balaamu; hasira yake
Balaamu ikawaka, akampiga punda kwa fimbo yake.
28
Bwana akakifunua kinywa cha yule punda, naye akamwambia Balaamu,
Nimekutenda nini, hata ukanipiga mara tatu hizi?
29
Balaamu akamwambia punda; Kwa sababu umenidhihaki; laiti ningekuwa na
upanga mkononi mwangu ningekuua sasa hivi.
30 Yule
punda akamwambia Balaamu, Je! Mimi si punda wako, nawe umenipanda maisha yako
yote hata leo? Nimezoea kukutenda hayo? Akasema, La!
31
Ndipo Bwana akafunua macho ya Balaamu akamwona malaika wa Bwana
amesimama njiani, ana upanga mkononi mwake, umekwisha kufutwa naye akainama
kichwa, akaanguka kifudifudi.
32
Malaika wa Bwana akamwambia, Mbona umempiga punda wako mara tatu hizi?
Tazama mimi nimekuja ili kukupinga, kwa sababu njia yako imepotoka mbele zangu,
33
punda akaniona, akageuka upande mbele zangu mara tatu hizi; kama
asingejiepusha nami, bila shaka ningalikuua wewe, nikamwacha yeye hai.
34
Balaamu akamwambia malaika wa Bwana, Nimefanya dhambi; maana sikujua ya
kuwa wewe umesimama njiani ili kunipinga; basi sasa, ikiwa umechukizwa,
nitarudi tena.
* wapendwa
katika mstari huu unaona jinsi Mungu alivyokuwa akiwatetea wana wa Israeli.
Ibilisi alitaka awashinde kwa njia ya uchawi lakini uchawi huo haukupata
nafasi. Swali kwanini Walipata ulinzi kiasi hiki? Kumbuka wana wa Israeli
walikuwa wana shida kama wewe? Waliomba kama wewe? Walifunga kama wewe? Na
Mungu aliwaahidi kuwatoa misri kwa wajumbe wa Mungu, kwa maono, kwa ahadi, kwa
maagano aliyoyafanya kwa neno kupitia Ibrahimu kama wewe ilivyo sasa haina
tofauti, Unavyosimamia mistari ya biblia kilichofanya Mungu awatoe ni baada ya
wao kutoa sadaka ya pasaka, kama jinsi walivyoelekezwa na Musa. Mpendwa
unapoomba vitu vikubwa katika ulimwengu wa roho,maombi ya ukombozi au
delivarence unapohitaji ufunguliwe kitu kikubwa lazima uambatanishe na sadaka,
sadaka manake ni kujiunganisha na madhabahu ya Mungu aliyehai. Lazima kiwepo
kitu cha kukuunganisha ulimwengu wa mwili na ulimwengu wa roho! Bwana Yesu
asifiwe!
Wapendwa
watu wa duniani wanapoenda kwa waganga au kutaka kukudhuru kwa uchawi wakienda
kwa waganga huwa wanaenda na sadaka mf. Ngombe 21, sadaka kubwa wanatoa ili
wewe ufungwe kiuchumi, ili wewe usifunguliwe ukapata mme, usipate kazi. Na
kadhalika wa kadhalika, watesi wetu sisi ni wachawi, ndio wanafanya maisha
yanakuwa yalivyo, nakueleza ili upate ufahamu wa Mungu,Sasa wengi wanasema Yesu
alifanyika sadaka kwetu mbele ya Mungu ni kweli lakini wewe umejiunganisha vip
na Yesu? Mungu alituumba sisi ni viumbe wake lakini alijiunganisha na sisi
kupitia sadaka ya mwanawe wa pekee. Kwa iyo Maombi makubwa yoyote ya ukombozi
muhimu kujiunganisha na sadaka. Najua unajua ila nakukumbusha uone umuhimu
wake. Pamoja na kufunga tatu kavu, pamoja na maombi yako. Chukua sadaka
iunganishe na
damu ya Yesu. Iunganishe na madhabahu ya Yesu ili ikakupiganie.
Bwana Yesu asifiwe. Wengi tunaomba alafu hatuna sadaka maalumu ya kujiunganisha
na maombi hayo maalumu. Au hiyo sadaka unaitoa tuu bila nayo kuiombea Bwana
Yesu asifiwe! Angalie ile sadaka ya pasaka ya wana wa israeli ilikuwa
inataratibu zake na siku yake. Ivyo usipeleke sadaka yako kavukavu kama
unaitupa pata mda wa siku hata moja kuifungia kuiombea kuitamkia, na kuiunganisha
na damu ya Yesu. Matokeo yake ni kama unayaona hapo juu kwenye neno, narudia
tena uchawi upo na ni vita yetu sisi tuliokoka kila siku.kazi ya uchawi ni
kukudhoodisha kwanza, kukupunguza makali yako ya imani au kuomba, kisha ndiyo
wanapiga, utauliza nimejuaje angalia hapo juu kwenye neno. Watu wa ulimwengu
huu wana maarifa kuliko sisi wa rohoni. Wanapeleka sadaka kubwa na kuiunganisha
na madhabahu zao za kukufunga wewe. Wanakufunga ufahamu,ndoa yako, kipengele
cha ndoa,uchumi,mikono yako ya uzalishaji, nyayo za miguu yako ya kumiliki,
wanakutupia mikosi balaa, kutokufanikiwa, kuzaa mapooza n.k Na wewe toa sadaka
kuiunganisha na damu ya Yesu na madhabahu ya Yesu. Kama kuna kitu umepata
mrudishie Mungu utukufu.
JINA LAKE
MUNGU LIBARIKIWE!
*kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka
nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako
biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni
kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige
hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande
wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi
ndugu yako Joseph Ntandu
josephntandu@gmail.com,0713297066
josephntandu@gmail.com,0713297066
Comments
Post a Comment