MSITENDE NENO LOLOTE KWA KUSHINDANA

Somo: Msitende neno lolote kwa kushindana

3  Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.

4  Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.

5  Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6  ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7  bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8  tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

 9  Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
 10  ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

 11  na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

 12  Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.

 13  Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.

 14  Yatendeni mambo yote pasipo manung'uniko wala mashindano,

Wafilipi 2.

*Bwana Yesu asifiwe, Leo asubuhi tuangalie roho ya mshindano jinsi inavyozuia Baraka za wapendwa. Roho ya mshindano ni roho wa ibilisi. Mashindano yanaleta chuki, 

mashindano yanaleta kijicho, mashindano yanaleta wivu, mashindano yanaleta kutaka kuonekana(roho ya yebesi), roho ya kujionyesha, roho ya kutaka kutambulika.


Roho ya kutaka kuabudiwa, roho ya kutaka kusifiwa, roho ya kutowadhamini watu wengine, roho ya kujikweza, roho wa kuwashusha wengine, inasikitisha kanisa siku hizi limeingia kwenye 

mashindano, baathi ya wazazi wetu wa kiroho kidogo baathi yao  wamepungukiwa na utukufu wa Mungu na kutaka kuonekana Wao badala ya kuonekana Yesu.


 Kiasi cha kuanza kuponda makanisa mengine, kuponda watumishi wengine,bila kujua huyu ni mtumishi aliyeitwa na Mungu au siyo! kitu kibaya Sana kumnyooshea kidole mtumishi ambaye kala gharama, ambaye Mungu 

kampaka mafuta sababu ya mashindano ya kimwili. Yesu atusaidie! Tabia hii imehamia mpaka kwa waumini kiasi cha kutoa sadaka kwa mashindano ya kuonekana sio kwa kusikia sauti ya Roho wa Mungu, mashindano yameingia 

mpaka kwenye mavazi kanisani, mashindano yameingia mpaka mtu anapopata nafasi ya kusimama mbele ya kanisa kutaka kutambulikana. Kufahamika. Yesu atusaidie!


Tumefikia sehemu ya kujitanguliza sisi kisha Yesu nyuma, Bwana Yesu asifiwe, kumekuwa Na mashindano hata kwenye utoaji wa neno, ufundishaji wa neno, kusifu na kuabudu, kuhubiri neno nia ya kwanza ni mtu binafsi apate sifa badala 

Yesu apate sifa. Hii huwa inaenda mpaka kwa waimbaji wa nyimbo za injili, utakuta akishapata nafasi tuu ya kuimba akimaliza kuimba anaondoka katika ibada au anaenda kukaa nje. Kana kwamba ile ibada haimuhusu tena. Bwana Yesu atusaidie.


Sehemu ambayo mtu anakuwa juu ya Yesu au juu ya Mungu, utukufu wa Mungu  hupungua mahali hapo, Neema ya Mungu haikai, maana nia ya Neema 

ya Mungu, utukufu wa Mungu, nuru ya Mungu kwa watumishi, au wapendwa ni ili utukufu umrudie Yesu. Yesu utusaidie!

 Mahali ambako Kuna mashindano katika kazi ya Yesu utukufu wa Mungu hupungua huondoka, mahali penye kufunga kwa mashindano, kutoa sadaka

 kwa mashindano, kuomba kwa mashindano, kuhubiri kwa mashindano,

 kufundisha kwa mashindano, kuabudu&kusifu kwa mashindano, kufanya ya Mungu kwa mashindano utukufu wa Mungu huondoka. Utukufu wa Mungu hukimbia.


Mungu hawezi toa matokeo makubwa kwenye mashindano, maana tokea mwanzo nia imebadilishwa imekuwa Na kusudi sio la kumtukuza Mungu. Kwa iyo

 utukufu haumrudii Mungu. Mungu sehemu iyo hatendi, hafanyi, anakaa kimya, sababu iyo Baraka, Neema, Nuru, utukufu wa Mungu utatumika vibaya 

upande wa ibilisi. Ni mpaka ujitambue, urudi kwa Mungu ndipo sasa atakuvusha. Swali la kujiuliza ndani mwako Kuna mashindano? Zipo 

chembechembe za kutaka sifa?,kutambulika?,kuoneka umefanya?, kabla ya Yesu? Huo ni ukuta mpendwa. Je unaposhauri mambo ya Mungu je 

unashauri kwa mashindano?unarekebisha kwa mashindano?  Sehemu unapoabudu Kuna mashindano? Mungu anaona kila kitu huwezi mficha chochote kila mahali yupo, hata ukienda kuzimu utamkuta.

 Lakufanya usiingie kwenye dhambi ingine usiinue mdomo wako kuanza kuongea kuhusu hayo mashindano, wala usijaribu kuhukumu.

Omba rehema, tubu kwa ajili yako, tubu kwa ajili ya kanisa, tubu kwa ajili ya waimbaji usiwahukumu, tubu kwa ajili ya mzazi wako wa kiroho usimnyooshee mtu yoyote  kidole, iyo ndio kama 

iliyokufunga kusababisha usipokee mda wote huu. Leo kweli imekuweka huru omba rehema mbele ya Mungu Baba kwa mashindano ndani yako, omba 

rehema kwa kufanya kusukumwa na mashindano, iyo ni kamba ya mauti, omba rehema kiri udhaifu wako kwa Yesu, Mwombe Yesu akusaidie ukivuka hapo. Yesu atakupa alichokuzuia sababu ya mashindano. Jina la Bwana libarikiwe. Amen


JINA LAKE MUNGU LIBARIKIWE!
 *kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu


josephntandu@gmail.com,0713297066






Comments

Popular posts from this blog

MAOMBI HATARI YA KUVUNJA UCHAWI WA MAFUNDO

MAOMBI YA KUFUNGUA KIBALI CHA  NAFASI YA KAZI

MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA KUCHELEWESHA