PART B ARDHI IMEBEBA ROBO TATU YA MAISHA YA BINADAMU



Part B

Somo: Ardhi imebeba roho tatu ya maisha ya binadamu.

*Baada ya kujifunza kuhusu madhabahu jinsi ambavyo inavyocontrol ulimwengu wa roho,kuhusu ardhi hasa sehemu tunazokaa au kuishi na jinsi Mungu anavyoweza kuwa establish madhabahu sehemu tunazoishi and what is happening baada

 ya kuistablish katika ardhi unayoishi! Na jinsi shetani ivyo ivyo anavyoweza iga na kujitambulisha kwa madhabahu kupitia ardhi. Na nini kinatokea, na umuhimu wa ardhi na maisha yako.


*sasa ni muhimu. Kuona Mungu mwenyewe alivyobomoa madhabahu za ibilisi. Same alivyofanya ndo jinsi wewe utaenda kufanya kwa msaada wa roho mtakatifu.

*Pls maneno yote yaliyowekwa hapa ufuatilie kwenye biblia yako na kufuatilia.contents na msisitizo wa maelezo kwenye somo hili utalipata utakapokuwa unasoma mistari ile ya biblia kwa kuirudia na kuirudia!

 Maelekezo yangu ni kukusaidia uelewe! Kama nilivyosema Ni somo sensitive, ivyo soma Mara ya kwanza ya pili utaanza kuelewa taratibu kupitia hayo maandiko,

 jinsi unavyosoma na kusoma ndivyo unazidi kufunguliwa na maelezo yangu kidogo. Ukielewa hapa jua kabisa umevuka kipande kikubwa Sana.

Waamuzi 6-11-16

11  Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani.

 12  Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa.

 13  Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu,

 waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je! Siye Bwana, aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani.

 14  Bwana akamtazama, akasema, Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani. Je! Si mimi ninayekutuma?

 15  Akamwambia, Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu.

 16  Bwana akamwambia, Hakika nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kama mtu mmoja.

* wote tunaifahamu habari ya Gedion na ninajua wote mnaipenda kama Mimi jinsi ninavyoipenda; 

*Baba yake Gedion alikuwa mshirikina na watu walikuwa wanakuja nyumbani kwa Baba yake Gedion kufanya mambo Yao.

*Mungu akaamua kumtumia Gedion ambaye ndo alikuwa mdogo kabisa Katika familia hii. Na akaamua kwenda kwenye ingini ya tatizo. Yani Ni sawa na sasa hivi awepo mshirikina mtaani kwenu alafu Mungu amtumie mtoto wa mshirikina kukomboa mtaa mzima. Bwana Yesu asifiwe!

*angalia pia hapo juu Gedion anamwambia BWANA kuwa Mimi ni mdogo na pia ni masikini nitawaokoaje wana wa Israeli? Kitu kimoja ambacho

 nataka nikumegee angalia Baba yake Gedion anamtumikia shetani na nyumbani kwake Kuna madhabahu ya ibilisi, lakini pamoja na hayo bado wakina Gedion ni masikini wakutupwa. Angalia hapo juu anavyomjibu Bwana. Labla ulitegemea

 wakina Gedion wawe na maisha mazuri sababu lango la kuzimu lipo kwao kwa iyo watu wanapokuja kuleta kafara zile au sadaka kwenye iyo madhabahu labla

 wangenufaika lakini ndo kwanza maisha yakina Gedion yanakuwa magumu zaidi. Ndo mana hata wachawi na waganga

 angalia maisha Yao.angalia maisha ya watoto Wao, angalia ndugu zao wa karibu utakuta wanakufa tuu. Au wanauana Si kitu mtu unaweza tamani hata kidogo.

*Sasa angalia Mungu anampa assignment Gedion ya kuvunja Madhabahu ya Baba yake mwenyewe,Na Baba yake hajui. maana ndio inayowaletea umasikini na taabu zote.

 Angalia mstari wa 13,mlango wa 6 kule juu. Gedion anamlalamikia Mungu kuwa yule Mungu tuliyemsikia kwa Baba zetu

 yako wapi matendo yake? Bila kujua sasa Mungu kaleta majibu. Yani kwa maana ingine anamwambia Gedion tatizo lipo

 nyumbani kwa Baba yako hapo unapoishi.maana ndiyo inayofanya Yale matendo makuu ya Bwana msiyaone. Ndio inayowalete umasikini wenu. Angalia mwenyewe hapo juu maandiko.

Mlango wa 6

22  Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gideoni akasema, Ole wangu, Ee Bwana MUNGU! Kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso.

 23  Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa.

 24  Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri.

 25  Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, Mtwae ng'ombe wa baba yako, yaani ng'ombe wa pili, wa miaka saba, ukaiangushe madhabahu ya Baali, aliyo nayo baba yako, ukaikate Ashera ile iliyo karibu nayo;

 26  ukamjengee Bwana, Mungu wako, madhabahu juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; ukamtwae yule ng'ombe wa pili na kumtoa awe sadaka ya kuteketezwa, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata.

 27  Ndipo Gideoni akatwaa watu kumi miongoni mwa watumishi wake, akafanya kama Bwana alivyomwambia; lakini ikawa kwa sababu aliwaogopa watu wa nyumba ya baba yake, na watu wa mji, hakuweza kuyatenda hayo wakati wa mchana, basi aliyatenda usiku.

 28  Hata watu wa mji walipoondoka asubuhi na mapema, tazama, madhabahu ya Baali imebomolewa, na ile Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na yule ng'ombe wa pili ametolewa sadaka juu ya ile madhabahu iliyojengwa.

 29  Wakaambiana, Ni nani aliyetenda jambo hili? Hata walipotafuta habari na kuuliza, wakasema, Gideoni, mwana wa Yoashi, ndiye aliyetenda jambo hili.

 30  Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi Mlete mwanao, afe; kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali na kwa sababu ameikata ile Ashera iliyokuwa karibu nayo.

 31  Yoashi akawaambia watu wote waliokuwa wakishindana naye, Je! Mtamtetea Baali? Au mtamwokoa ninyi? Yeye atakayemtetea na auawe hivi asubuhi; kama yeye ni Mungu, na ajitetee nafsi yake, kwa sababu mtu mmoja ameibomoa madhabahu yake.

*Sasa hapa tunakuja jinsi kubomoa tatizo, nikupe kitu kimoja unapo okoka Ni tiketi ya kwenda mbinguni. Ila kufanikiwa hapa duniani ni vita ingine lazima upigane bila kuchoka. Katika kupigana ndipo Bwana

 atakuja kukusaidia kukutoa. Jiulize kama Bwana asingelimtokea Gedion hivi angejuaje kama matatizo yote kumbe yapo nyumbani kwako. Tena kwa Baba yake? Can you imagine? Unaenda kanisani  huko mnakesha kuomba, unamtafuta

 Mungu kwa gharama kubwa mno kumbe tatizo lipo nyumbani kwako. Kumbe tatizo lipo kwenye Shamba la Babu yako huko kwenu. Kumbe nyie mlikabithiwa kwa mizimu. Mwingine atasema lakini si nimeokoka ni sawa. Kumbuka Yesu

 ilimbidi Angie ardhini afe afufuke ushawahi jiuliza kwanini Yesu alizikwa ardhini? Leo ngoja nikujibu Yesu alizikwa ardhini ili kuharibu madhabahu zote ziliwekwa na ibilisi katika ardhi. Ushawahi sikia wakisema nchi ya Israeli ukienda kule

 ukikanyaga unasikia uwepo wa Mungu? Ushawahi jiuliza kwanini? Ni sababu ile ardhi imetengenezewa madhabahu. Kitendo cha Yesu kutoka Katika ukoo wa Ibrahimu na Daudi kimemuunganisha na ardhi ya Israeli. Kwa iyo yeye kufa na kuzikwa katika ardhi manake Ni

 kukamilisha madhabahu katika Israeli ndo mana kuna uwepo wa Mungu. Yesu alikuwa anajenga madhabahu pale kaivari. Bwana Yesu asifiwe.By the way Shetani anaiga kila kitu. Angalia jinsi Yesu alivyosulubiwa na kufa na kuzikwa. Haina tofauti

 wanavyochukua mnyama kumchinja na kumfukia katika ardhi.sema kinachotofautisha ni lango lipi? Shetani anaiga tuu. Bwana Yesu asifiwe watu wa Mungu. Ninaongea haya ili macho yako yafunguke. Na ukifunguka wewe utawafundisha wengine.


*Sasa angalia maelekezo ya Mungu Gedion aliyopewa ili kuangusha madhabahu za baali. Ooh Jesus i love your bible! Ni nzuri! Mungu akamwambia achukue ngombe wawili, ngombe wa kwanza ni wa kuangusha madhabahu ya Baba yake.

 Ngombe wa pili ni kumjengea Mungu madhabahu. Soma kwa makini mstari wa 25,26,27,28! Niliposema neno hili ni sensitive angalia jinsi kiti cha enzi cha

 shetani Mungu alivyokingoa. Kwa utaratibu! Gedion pengine angekosea maelekezo pengine angekufa. Sababu usifanye mchezo na madhabahu.

*Sasa Gedion kwa kuona ile hatari alivunja ile madhabahu usiku na walipoaamka wakakuta madhabahu hakuna tena. Angevunja mchana ingemletea shida.

*Sasa hapa ndipo patamu baada ya ile madhabahu kuvunjwa  mstari wa 29, wale wachawi, waganga, wapiga ramli, ma urgent wa ibilisi wakajiuliza ni nani aliyebomoa madhabahu hii? Walipotafuta

 wakaja gundua Ni Gedion mwana wa Yoashi, sasa angalia mstari 30! Yoashi ndo alikuwa mkubwa wa Ile madhabahu ya ibilisi na sasa wale waabudu baali wanamfuata Yoashi wanamuambia mtoe

 mwanao auawe! Sasa hapo ndipo lile neno  somo la Kwanza ufunuo 11-7 utaliona, kuhusu yule mnyama aliyepewa nguvu na ibilisi na kiti cha enzi, na nguvu nyingi. uyu ndo anasukuma watu sasa wakamuue Gedion. Lakini Sababu sasa ile madhabahu haipo haina nguvu ndo mana Baba yake

 mwenyewe Gedion, mstari wa 31 anawajibu "Mtamtetea baali? Au mtamwokoa ninyi? Yeye atakayemtetea auawe hii asubuhi!anasema kama yeye ni Mungu ajitetee nafsi yake" halleluyah halleluyah! God is Good. Angalia baada ya

 kuvunjwa madhabahu yule mkubwa wa wachawi ndio anawageuka wenzake anawaambia uyu mungu baali tuliyokuwa tunamwabudu kama yeye ni Mungu ajitetee mwenyewe, manake alikuwa anasema hivi ni Mungu gani uyu ambaye binadamu mpaka washike marungu na

 mapanga wamteteee! Mungu gani asiyeweza jitetea. Kwa maana ingine Mungu akanionyesha kitu angalia jinsi mungu wa ndugu zetu waislamu kwanini wanafikia sehemu wanatumia upanga au kujilipua na mabomu kulazimisha sheria zao je maombi Yao hayatoshi?

 Inamaana ni mungu ambaye hawezi kujitetea ndo mana wanamtetea kwa nguvu zao. Ni Mungu wa aina gani anayetetewa na watu? Mungu anatakiwa atetee watu. Sio watu wamtetee kwa kumpigania vita. Vita vinafanywa na mungu na sio na watu Bwana Yesu asifiwe

 ndio maana sisi Mungu wetu anajitetea mwenyewe. Bwana Yesu asifiwe Sana.  Inamaana kama ile madhabahu ingalikuwa haijavunjwa pengine Baba yake angemnyonga mwenyewe mwanae. Maana lile joka la ibilisi lingemwekea

 hasira  ndani ya Baba yake. Bwana Yesu asifiwe Sana.na ivyo ndivyo jinsi Gedion alivyowaokoa wana wa Israeli kutoka Katika mateso ya mungu baali.

*mpendwa nachotaka kukuambia ni hiki kila tatizo linaufumbuzi wake. Kama ulifungua kipengele cha uchumi kwa kutumia upako mafuta wa mafuta ya Mtumishi flani haina maana pia

 unapotaka kupata watoto lazima Mungu atumie hayohayo mafuta. Bwana Yesu asifiwe Sana. Inawezekana kabisa shida unayopitia inatokea kwenye ardhi.vita vya miungu. Sisi hatuchinji ila isipokuwa tunatumia damu

 ya Yesu ambayo ilishaandaliwa kwa ajili ya wewe kutumia. Kuiombea ardhi tunaiombea kwa kuishika tuu.ardhi asili yake inalaana rejea stori ya kaini kitabu  cha mwanzo. Lakini laana ile vunjwa na Yesu. Halleluyah. Ila hata baada ya ukombozi wa ardhi bado binadamu wameendelea kumjenge ibilisi madhabahu kupitia ardhi hapo ndipo tatizo linapokuja sasa. Na kujua unachokifanya. Baada ya kuelewa sasa.

Sasa twende jinsi ya kuiombea ardhi. Hapa nazungumzia ardhi ya maisha yako. Unapoishi, ulipowahi kukaa, ardhi ya kwenu, kabila la mama yako, kabila la baba yako, ardhi hii ikifunguka na vitu vingi Sana vitafunguka. Na unapoanza

 maombi haya usiache! Ila tuu nikujulishe vita lazima vitakuwepo ila Ni bora kupambana kwa Maombi ili ufanikiwe kuliko kubaki kwenye vifungo unaenda mbinguni na umasikini wako na vifungo

 vyako. MUNGU ATAKUSAUDIA UTASHINDA.Ardhi hii unachukua kidogo tuu mkononi unaomba. iyo iyo hapo unapoishi unaishika kwa kutumia ardhi ya kwenu kwa imani. Yani ardhi mkoani kwenu unaishika kwa imani. Kumbuka ulimwengu wa roho hakuna umbali. Kumbuka yule akida akamwambia Yesu sema neno moja tuu. Ili ujue kuwa katika ulimwengu wa roho hakuna umbali. Na dunia hii hata kiganjani kwa Mungu haitoshi. katika Yale mambo yako magumu embu yafungue kupitia ardhi.

Mtumishi mmoja anasema alipoanza kuiombea ardhi ya kwao kule machame moshi akaanza kuota wanyama wa kutisha anapambana nao. Kumbe kwao Kuna makaburi si unajua wachagga makaburi yanakuwa nyumbani kwa mtu. Akawa anaamshwa usiku Sana anaomba. Baada ya kuomba

 mda si mrefu akaja akaota limetokea dubu na Chui wanamua attack lakini katika vita ivyo Mara wakageuka watu wenye upanga mrefu Sana, wakataka kumkata, akashika ule upanga akausukumia shingoni mwake akamchinja wakafa. Na baada ya hapo alipata ushindi mkubwa

 Sana anasema Kuna mahali alikwama kabisa akavuka kiurahisi. Mama mwingine arusha alikuwa akilala anatambaliwa na wadudu sisimizi hawaoni lakini wakamuombea miaka na miaka hajawahi

 pata nafuu lakini watumishi walipoenda kuiombea ardhi wale sisimizi Mtumishi anasema aliwaona kwenye ndoto wanaanguka wanakufa ndio uponyaji wa uyo mama.

*kwa iyo Roho mtakatifu akikusukuma Leo au baadae ufanye maombi haya yafanye. Ila akikuambia subiri basi subiri.

Sasa twende kwenye hatua ya mwisho 



Hatua 10 za kuiombea ardhi

(according to Roho Mtakatifu alivyonifunulia)

*Maombi yawe ya siku 7, na muendelezo mpaka umevuka na kupata ushindi. Muhimu kufunga masaa 12, kufunga manake kuruusu ulimwengu wa roho uwe active zaidi ya mwili. Uwe katika mood ya kuomba mda wote.

1.Jitakase kwanza wewe mwenyewe kwa damu ya Yesu. Omba uongozi wa roho mtakatifu katika maombi haya. Omba ulinzi wa Mungu kwako kwa damu ya Yesu juu ya Maombi haya. Isaya 54:17

2. Watakase watu wote waliohusika kujenga madhabahu kwa damu ya Yesu. Hata kama huwajui achilia damu ya Yesu juu Yao watatakasika na kuwekwa huru. Isaya 1:18. Damu ya Yesu inamacho Saba (7) na roho Saba (7) damu itawafuata na kuwatakasa. Hata kama hawapo ila madhara yake yaliyobaki kwa watu yatatakaswa kwa damu ya Yesu. Usicheze na hii damu kabisa.

3. Shika ardhi mkono wa kuume omba rehema kwa ajili ya ardhi iyo. Itakase iyo ardhi kwa damu ya Yesu, futa laana zote zilizotokana na kafara, madhabahu za ibilisi omba rehema kwa iyo ardhi kwa kutumia kama malango ya kuzimu. Achilia damu ya Yesu juu ya iyo ardhi. Utakaso na uponyaji.

4. Sifu na kuabudu huku umeshika iyo ardhi ili isikie nyimbo za Mungu. Ardhi huwa inasikia. Abudu na kusifu mpaka mzigo huo umeisha ndani yako. Kwa kufanya ivyo unakaribisha uwepo wa Mungu Katika iyo ardhi.

5. Anza kubomoa sasa na kuharibu kwa damu ya Yesu madhabahu zote zilizojengwa na ibilisi, na kungoa viti vya enzi kwa mamlaka ya jina la Yesu, na kwa damu ya Yesu huku umeishikilia ardhi.

6. Kwa damu ya Yesu sasa na mamlaka ya Yesu shusha kiti cha enzi cha Yesu Katika iyo ardhi, ruusu sasa makao ya kiti cha Yesu Katika iyo ardhi. Huku umeishika iyo ardhi.

7.Jenga sasa madhabahu ya Yesu. Unganisha iyo ardhi na madhabahu ya msalaba wa Yesu. Unganisha iyo ardhi kwa damu ya Yesu na madhabahu ya Yesu aliyoijenga pale msalabani. Amuru uhai tokea ardhini wa Yesu ule ulioshinda mauti uje katika ardhi uingie katika iyo ardhi kwa jina la Yesu.

8.Mshukuru Yesu kwa yote mpaka sasa. Utakuwa umefanya jambo kubwa Sana katika ulimwengu wa roho. Ingawa kwa macho huoni ila amini inatendeka kwa 100%. Shetani asije kukudanganya eti hakuna kitu. Inafanyika.

9. Sasa ni mda mzuri wa kutamkia mema iyo ardhi, kupitia iyo madhabahu uliyoishusha sasa jenga upya vitu vyote vilivyoharibika, fungua malango ya kifamilia na ukoo yaliyofungwa katika iyo madhabahu ya Yesu. Fungua mambo yako binafsi pia yaliyofungwa au ambayo hayaendi kupitia iyo madhabahu ya Yesu. Tumia damu ya Yesu kutamka.

10. Toa sadaka ya shukrani ya maneno, katika iyo madhabahu ya Yesu. Toa sadaka ya shukrani dhabihu ya kumshukuru Yesu kwa kujenga madhabahu mpya katika iyo ardhi. Hakuna madhabahu ambayo haitolewi sadaka.  Sasa kwa sadaka iyo Eneenee kwa damu ya Yesu kupitia iyo madhabahu uombe Yesu akupiganie endapo Kuna vita vyoyote vitainuka kwa sababu ya kungoa viti vya enzi vya ibilisi. Na kwa sadaka iyo uliyoiunga kwa damu ya Yesu. Omba Yesu afungue mipango yote iliyokuwa imefungwa.

*mpaka hapo unaushindi mkubwa Sana. Jina la Bwana libarikiwe.

*kumbuka tunaombea ardhi ili kufungua mambo yaliyokuwa yametufunga. Na kuleta ufalme wa Mungu mahali unapokaa. Ivyo baada ya Maombi haya utaendelea na Maombi yako ya kila siku. Bwana Yesu asifiwe Sana.

*Pia hata siku Saba zikiisha tokea Leo weka utaratibu wa kuendelea kufungua ardhi. Jinsi inavyofunguka ndivyo jinsi Kuna mambo ilikuwa huyaoni utaanza kuyaona. Na utaanza sikia Mungu kwa clear akiongoe.

*Ibilisi asikudanganye eti hakuna kitu no kipo kitu. Ni janja ya kukufanya uache kuomba.

Nikutakie ushindi mkubwa katika maombi haya Katika jina la Yesu.

kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu

Comments

Popular posts from this blog

MAOMBI HATARI YA KUVUNJA UCHAWI WA MAFUNDO

MAOMBI YA KUFUNGUA KIBALI CHA  NAFASI YA KAZI

MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA KUCHELEWESHA