TEKETEZA ROHO ZINAZOPOFUSHA NENO LA MUNGU
Tuangalie
neno kwa kifupi
Tokea Leo hii jua ya kwamba Kama huwezi soma biblia
inasoma vipande vipande vya mstari basi unapambana na nguvu za Giza za
kupofusha akili za watu, Kama hulielewi neno jua ni ibilisi, Kama huna mda wa
kusoma neno jua ni ibilisi, Kama hamu ya kusoma inakatika
Somo: "Teketeza roho zinazopofusha neno la
Mungu"
Matendo 13-6.....
Mpendwa neno la Mungu limehakikishwa Mara saba, ni
taa pale kwenye Giza, ni upanga ukatao kuwili, kazi yake kukata kufyeka ya
ibilisi. Ndani ya neno Kuna nguvu kubwa Sana ya kujenga, kubomoa, kila kitu
hapa duniani kilitokana na neno la Mungu, neno ni silaa, neno Lina nguvu kuliko
kitu chochote hasa neno
litakalo na Mungu. Neno la Mungu katika biblia
linachunguza moyo wako, linahuisha, linatafsiri, linaongea Yale ya Mungu kwako,
linaleta maono, neno la Mungu Lina maelekezo ya Mungu. Kila kitu kimefichwa
kwenye neno, kila shida na taabu hapa duniani jibu lake limefichwa katika neno,
ndio maana ibilisi hufanya
mbinu zote ili kupofusha akili za watu, kupigana nao
wasije wakasoma biblia hata wakisoma wasielewe, wakielewa wasiamini, neno
linapisomwa linapokaa moyoni humzuia ibilisi kufanya kazi,
katika maisha yako,
roho mtakatifu hawezi ongea mambo ya kimungu au mafumbo ya Kimungu katika
maisha yako maana huwezi lielewa ni mpaka uwe na neno katika moyo wako. Mungu
watu wengi haongei nao jumbe nzito direct
na Wao maana hawana neno la kutosha,
vifua vyao ni vidogo, bado hawako tayari, mtu wa ndani kusudi afanye kazi
kiwango kinachotakiwa lazima umlishe neno, umpe chakula cha kutosha, muhimu
kupata mda binafsi wa kusoma biblia, watu wengi Sana huwa wanalalamika
wamechoka kiroho, wamechoka majaribu,
maombi yamekauka, lakini ukichunguza neno
aliloweka katika moyo wake ndilo lililotumika kumpigania. Lakini ukiwa na neno
la kutosha hutasinyaa, wala kuchoka kiroho, mambo ya hapa duniani
hayatakuchosha moyo wako, neno
linapojaa kwa wingi vitu vya nje au vya duniani
haviwi tena ishu, tena neno linaondoa hofu, wasiwasi mashaka, linaleta amani na
furaha ya kweli. Lakini ipo vita katika kufikia uhuru wa kusoma neno,
ivyo
nilitaka kukuonyesha hata biblia imezungumza kwa habari ya uchawi wa kuzuia
wewe usilipende neno, usiliamini neno, ndo mana ni muhimu kujikabithi kabla ya
kusoma biblia yako, kabla ya kuanza ibada au seminar mwambie Mungu nataka
nitoke na kitu changu. Kukemea roho za kupofusha akili, roho za kuzuia
wewe
kuamini. Maana utakapolisikia neno na kuliamini na kuliweka katika matendo hata
wakati wa majaribu hakika utaokolewa, biblia inasema walitialo jina la Bwana
wataokoka.
6
Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu
mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;
7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio
Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake,
akataka kulisikia neno la Mungu.
8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo
tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha
ile imani.
9
Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia
macho,
10
akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa
haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?
11
Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione
jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta
mtu wa kumshika mkono na kumwongoza.
12
Ndipo yule liwali, alipoyaona yaliyotendeka, akaamini, akiyastaajabia
mafundisho ya Bwana.
Ibilisi akitaka akucheleweshe katika miujiza yako,
atapigana na wewe katika neno katika kusoma neno, ni vizuri kwenda katika
maombi kufunguliwa for delivarence, au maombi ya ukombozi. Ni vizuri kutumia
mafuta yaliyoombewa, ni
vizuri kutumia maji yenye upako yaliyoombewa, ni vizuri
kuwekewa mikono lakini amini usiamini kupokea kwako kunategemea kiwango cha
neno na imani iliyojengenga ndani yako, bila neno hutaweza pita kwenye
maandalizi ya wewe kupokea ya Mungu, bila neno utaanguka katika dhambi kila
Mara, bila neno utazunguka makanisa yoote kwenda kuombewa lakini amini usiamini
bila neno hata iko unachopokea kitadumu kwa Mda tuu. Maana ni jukumu lako
kukitunza kwa imani, Si akili zako za duniani.
Halleluyah! BWANA Yesu asifiwe,
matatizo yote unayaona katika akili ya ufahamu wako, ni uongo ulijengwa na
ibilisi, ivyo bila neno hakuna lolote utakalofanikiwa. Hatuna ujanja. Tenga mda
wako wa kusoma neno,
jijengee imani yako, Si kila Mara imani ya mtumishi
itakusaidia wewe, Tenga mda wako kwa ajili ya kusoma biblia. Hii injili ya
pokea! Pokea! Ni nzuri lakini pasipo neno la imani ni kujifirahisha tuu nafsi
yako. Halleluyah! Jiongeze!
Ufahamu wako, sikiza watumishi mbalimbali, kupata
vyakula tofauti tofauti, ongeza kiwango, komaa kiroho. Kitu chochote mtu
anacholalamika analalamika ni sababu neno halijakaa vizuri ndani kwake.
au huna kabisa jua ni
ibilisi, wakati wewe ukivunja na kuangamiza kwa jina la Yesu, ni kweli
inatendeka lakini yeye atakubania kwenye neno ili matokeo yako yawe
madogomadogo tuu, atakuzuia kiwango chako cha neno, atapigana na wewe kipengele
cha neno, maana ukifunguka hapo wewe ni mshindi. Usikubali kupigwa eneo la neno, ni sehemu ambayo unatakiwa umwombe Mungu kila siku kipengele
cha neno, maana ukifunguka hapo wewe ni mshindi. Usikubali kupigwa eneo la neno, ni sehemu ambayo unatakiwa umwombe Mungu kila siku kipengele
cha neno,
mpaka pale utakapokuwa huru kabisa. Kusoma neno kwa kulipenda. Kulimiss
unapokosa biblia uone kiu. Silaha ya kwanza kabisa ni neno kukaa kwa wingi
ndani yako. Si kweli huna mda, iyo pia ni vita ya ibilisi, utalia na Baraka kwa Mda mrefu baada ya mda inatoweka, kwani hujawahi ona au expirience? Kama ni ela inakatika, ukichunguza shetani alianza
ndani yako. Si kweli huna mda, iyo pia ni vita ya ibilisi, utalia na Baraka kwa Mda mrefu baada ya mda inatoweka, kwani hujawahi ona au expirience? Kama ni ela inakatika, ukichunguza shetani alianza
vita ndani ya moyo wako, sababu kulikuwa
wazi ndo mana kakushinda. Message hizi ni ngumu na Si kila mtu hufuraia, lakini
lazima tuseme ili mtu wa ndani apone. Jina lake Mungu libarikiwe
JINA LAKE MUNGU LIBARIKIWE!
*kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu
josephntandu@gmail.com,0713297066
.
Comments
Post a Comment