UKUTA UNAOZUIA BARAKA



 Somo: "Ukuta unaozuia Baraka"

Bwana Yesu asifiwe Sana!

Yohana 8-31-32

31  Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;
 32  tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.

Ninyi MKIKAA ndani YANGU na maneno yangu YAKIKAA ndani YENU. mmekuwa WANAFUNZI wangu KWELI KWELI mmekuwa wanafunzi. Tena MTAIFAHAMU KWELI, nayo hiyo KWELI itawaweka HURU

Leo tunazungumzia ukuta wa Baraka, Kuna njia ya Baraka na ukuta wa Baraka, wengi hatumalizii homework, njia ya Baraka tunaijua na tunaifuata, kupanda mbegu tunapanda, tunakesha tukiomba, tunafunga, tunatoa sadaka kwa yatima, tunasupport kazi ya Mungu, matendo mema kwa wengine, tunafanya huduma ya Mungu. Well done! Na mambo yoote kabisa. Izo ni njia za Baraka, tunatoa fungu la kumi (10) kuongezeka. Tunatoa malimbuko kupata ulinzi Bwana Yesu asifiwe Sana. Tunakumbushana tuu! Biblia ni kukumbushana alafu roho mtakatifu katika kukumbusha anasema kitu kingine, njia ingine anaongeza kitu kwenye ufahamu wako. Bwana Yesu asifiwe Sana.

Kwanini Baraka zinachelewa? Au zinakawia?

Kutoka 13:17-18

17  Ilikuwa hapo Farao alipokwisha kuwaacha watu hao waende zao, Mungu hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri;
 18  lakini Mungu akawazungusha hao watu kwa njia ya bara kando ya Bahari ya Shamu; wana wa Israeli wakakwea kutoka nchi ya Misri hali wamevaa silaha.


*Baada ya Mungu kukubariki kwa kawaida ndiyo mwanzo ya vita mpya! Just imagine mtu kasota kwenye magoti miaka minne (4) baada tuu ya kupata kazi miezi 6 mtu uyouyo, unasikia anataka kuacha kazi?unasikia hii kazi basi! Bora nitafute kitu kingine, Unajiuliza why? Mtu kasota anatafuta angalau aolewe au aowe! Baada ya mwaka mmoja tuu anataka kutengana unajiuliza amekuwa akimuomba Mungu miaka 5, Mungu kufanya vile anavyotaka hataki tena why?


Mtu naomba biashara (mtaji) kwa Muda mrefu Sana baada tuu ya kupata iyo biashara unasikia hii biashara naifunga! Unajiuliza why? Mwingine analia na watoto Hana mtoto. Baada ya kupata tuu mtoto akishaanza kukua Tuu anamlaani yule mtoto. Afadhali Mungu nisingekuwa na uyu mtoto, maana amegeuka mwiba,ananitesa, ananipandisha Bp, ananiletea uchungu kwenye moyo. unajiuliza why anatamka maneno kama haya kwa tatizo la kawaida kabisa? Dogo kabisa? Kwani watu baada ya Baraka tuu, wanakimbilia ku quit, hawataki tena why? Ndipo hapo ilo neno linakuja "wasije wakaghairi hawa watu watakapokutana na vita" kutoka 17.Mungu hukuzungusha njia ya kufika ili kukuandaa! Anajua moyo wako mdogo, imani yako ndogo, anajua hujakomaa kiroho kitu kidogo  unataka kumuacha Mungu.


Mungu anajua bado unakunywa maziwa hujaanza kula vyakula vya watu wazima katika wokovu. Mungu anajua nafsi yako ikiinamishwa na wachawi huwa unakata tamaa, unatamani kufa, huwa huwezi Ata kuomba. Mungu anajua moyo wako mdogo hauwezi kuhimili vita maana utakimbia.Mungu anakujua madhaifu yako. Anakujua wewe Ni mwoga si jasiri,anajua wewe Una aibu, aibu ni ukuta wa kufanikiwa, huwezi hata kuongea mbele za watu,anajua wewe ni mwoga, wewe huwezi kusema ukweli mbele unapotakiwa. Huwezi kutete haki maana Una huruma Sana. Mungu anakujua.Mungu anakujua wewe ni mtu wa kupanic ovyo. Na ukishapanic huna control tena ya akili yako. Mungu anakujua kabisa.


anajua wewe huwezi simamia watu katika kazi,maana huwezi kutoa Order unawaogopa watu,macho ya watu wewe unaogopa,  ajua wewe huwa unasusa ovyo, unazira ovyo, anajua wewe unachowaza ni kukimbia tatizo na sio kudeal na tatizo, anajua wewe huwezi kucontrol hasira, huna uvumilivu, Si msiri,mwingine Ni mwoga hata wa kuendesha gari tuu hajiamini alafu unatajka Mungu akupe hotel inayoingiza mil 10, kwa mwezi utaicontrol vip sasa?  ivyo anakurekebisha hatua kwa hatua ili ufikie kiwango kinachokibalika ili ufanye vita. Yes hapa duniani Ni vita mda wote. Mungu hakuandai ili ukalale ustarehe anakuandaa ili ufanye vita.


Ushinde wachawi, wanga, wapiga ramli, wasoma nyota, wachukua nyota, ushinde falme za Giza, ushinde wakuu wa Giza, ushinde mizimu ya ukoo inayokufuatilia Bwana Yesu asifiwe. Bwana anakutaka uwe chombo cha kupuria, uwe upanga wa kukatia, usitishwe usifadhaike. Uwe jasiri kuharibu kazi za ibilisi maana ndicho alichosema katika Yeremia 1:10. Akikupa unachotaka na bado hujavuka katika mifano huko juu utaharibu tuu. Misukosuko kidogo ikija utakimbia! Ndoa utaharibu! Mke utamkimbia! Mme utamkimbia! Kazi utaacha! Biashara utafunga! Huduma utaaicha! MUNGU anajua kila kitu bana. Ivyo unapochelewa wewe mshukuru Mungu tena mwombe Mungu akupe ukaribu na yeye! Yani jinsi ambacho hupati unachokiomba uwe sababu ya wewe kumsogelea Mungu umbali wa zero distance! Sio kukaa mbali Na Mungu au kuchukua shortcut unapofanya hivyo ndio unazidi kujichelewesha Bwana Yesu asifiwe!  Hakuna njia nyingine shetani nia yake Ni kukuingiza kwenye shimo Hana urafiki na wewe! Wewe utaona ni fahari ya mda ila mwisho wa siku lazima akutumbukize kwenye shimo alafu atakucheka.

Nini ni ukuta wa Baraka?
 
Mwanzo 4- 2-12

6  Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
7  Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
8  Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani,Kaini akamwinukia Habili nduguye,akamwua.
 9  Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?
 10  Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
 11  Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
 12  utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.

*WIVU
Watu wengi wanajidanganya Sana na matendo mema ya nje! Mungu huangalia nia ya moyo, Mungu huijua Ni ya moyo! Ukuta mkubwa mmoja wapo ni roho wa wivu, kumuonea wivu mwenzako Ni laana ya kutokufanikiwa, soma hapo juu Kaini alilaaniwa, kijicho pia kinakuleta laana ya kutokufanikiwa, mwingine anamwonea wivu mpaka Mchungaji wake anavyovaa, au mama Mchungaji anavyovaa, mtu akipendeza anamuonea wivu-kijicho anakasirika kama kaini soma hapo juu. Ukitaka kujua Kaini alikasirika Na kughadhibika angalia anavyomjibu Mungu alipoulizwa ndugu yako yupo wapi? Anamwambia Mungu Mimi ni mlinzi wa Habili? Je kweli unaweza mjibu Mungu kama binadamu kama siyo aliongozwa na hasira?

 Watu wengi wanamuonea Mungu wivu kwanini umembariki yule kwanini sio Mimi? Kwanini umempa biashara yule? Kwanini Mungu yule umempa gari? Kwanini umemfanya mkurugenzi, kwanini kampuni inamuamini anacontrol fedha zote, Je Mungu Mimi Na yeye kunatofauti gani? Watu wengi wanamuonea Mungu wivu na kumkasirikia kwa nini kabariki wengine na sio Wao? Kwanini uyu anamaisha mazuri na Sio Wao! Sasa hii ni mtego na wengi wanaona Ni kitu cha kawaida soma pale mstari wa 7 " usipotenda vyema dhambi iko inakuotea malangoni kwako nayo inakutamani wewe, yakupasa uishinde" Bwana Yesu asifiwe unapotenda wivu dhambi ii malangoni pako, inakutamani wewe, umeona laana inapotoka wapendwa. Juhudi zako zote zinafutwa na wivu.maana wivu huja na ghadhabu, hasira na chuki. Angalia pia situation mzima Mungu anaongea baada ya watu hawa kutoa sadaka kama wewe unavyotoa ili kufungua mlango wa Baraka, haina tofauti. Mwombe roho mtakatifu akujaze nguvu zake ili wivu huo kwa watu na kwa Mungu usiwe ukuta wa Baraka zako.

Mwanzo 25:29-34
29  Yakobo akapika chakula cha dengu. Esau akaja kutoka nyikani, naye alikuwa amechoka sana.
 30  Esau akamwambia Yakobo, Tafadhali, unipe hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo walimwita jina lake Edomu.
 31  Yakobo akamwambia, Kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza.
 32  Esau akasema, Tazama, mimi ni karibu kufa, itanifaa nini haki hii ya uzazi?
 33  Yakobo akamwambia, Uniapie kwanza. Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza.
 34  Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.

*KUUZA BARAKA
Watu wengi tunauza Baraka, kwa kujua au bila kujijua, Yohana 10:10 inasema shetani haji ila aibe, auwe, aharibu, achinje. Sasa kuibiwa huku usifikiri ni fedha kuibiwa huku ni pamoja na Baraka zako. Shetani hukutamanisha dhambi, na wewe ukishaitamani unamuuzia kwa kubadilishana naye! Anakupa hasira na wewe unampa Baraka, anakupa kutokusamehe na wewe unampa Baraka. Anakupa hongo na wewe unampa Baraka, anakupa kulipisha kisasi na wewe unampa Baraka, anakupa kiburi na wewe unampa Baraka, anakupa pombe, uasherati, uzinzi, Mali ya uwizi, utapeli, na wewe unampa Baraka, anakupa uongo na wewe unampa Baraka, anakupa chakula cha mda, na wewe unampa Baraka, Kuna tofauti ya Baraka na vitu. Isaka, yakobo, Mungu aliwapa Baraka yani Lango hawakupa vitu. Vitu huwa vinaisha lakini Baraka huwa haishi, vitu ni magari, nyumba, fedha iliyoko bank. Vikiondoka huwa vimeondoka. Wakristo wengi huwa wanaomba vitu kwa Mungu huwa hawaombi Baraka. Baraka haishi. Baraka linafanya lango kila linapokuwa halina ukomo, haliishi. Wengi Leo shetani anakupa vitu alafu anaondoka Na Baraka zako. Ulijua njia ya Baraka lakini Leo umejua ukuta wa Baraka. Na ili uache kumpa shetani Baraka na wewe ukabaki na vitu. Ndicho alichokifanya Esau alimpa Baraka Yakobo yeye akachukua kitu. Embu tuangalie Biblia

MWANZO 27:27
27  Akakaribia akambusu. Naye akasikia harufu ya mavazi yake, akambariki akasema, Tazama, harufu ya mwanangu Ni kama harufu ya shamba alilolibariki Bwana.
 28  Mungu na akupe ya umande wa mbingu, Na ya manono ya nchi, Na wingi wa nafaka na mvinyo.
 29  Mataifa na wakutumikie Na makabila wakusujudie, Uwe bwana wa ndugu zako, Na wana wa mama yako na wakusujudie. Atakayekulaani alaaniwe, Na atakayekubariki abarikiwe.

*Angalia hizo Baraka na kile chakula alichokula Esau je vinalingana? Vina dhamani? Tokea Leo acha kuuuza Baraka zako.

Nawe utaijua kweli. Na iyo kweli itakuweka huru. 

 
*kama hujaokoka ndugu chukua uamuzi leo umpe Yesu maisha yako. Kuokoka nikukubali Yesu atake control ya maisha yako ya kiuchumi,ndoa,kazi zako biashara zako, maisha yako ya kiroho, na mambo yote ya kiujumla, ni kumruusu Yesu atake charge ya maisha yako.kumruusu roho wa Mungu apige hatua na kuokoka si kubadili dini. Huwezi mshinda adui ukiwa upande wake,Hivyo chukua hatua leo ndugu, ukae upande salama kwa Yesu. Mimi ndugu yako Joseph Ntandu


josephntandu@gmail.com,0713297066

Comments

Popular posts from this blog

MAOMBI HATARI YA KUVUNJA UCHAWI WA MAFUNDO

MAOMBI YA KUFUNGUA KIBALI CHA  NAFASI YA KAZI

MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA KUCHELEWESHA